Menu
in , , , ,

Ronaldo ang’ara Real wakiwapiga Schalke

Cristiano Ronaldo amerudi kwenye kiwango chake baada ya kufunga bao muhimu na kumtengea Marcelo kufunga la pili katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL) baina ya Real Madrid na Schalke.
Wadau walikuwa wakihoji utimamu wa Ronaldo na kiwango chake cha soka kabla ya mechi hiyo, lakini ameonesha bado yumo.

Kocha wake, Carlo Ancelotti alimsifu akisema nyota wake huyo huishi kwa mabao.

Real sasa wameshinda mechi 10 mfululizo za UCL huku Ronaldo akifikisha mabao 58 kwenye mechi 58. Alikuwa amecheza mechi tatu bila kufunga bao.

Katika mechi hiyo iliyochezwa Gelsenkirchen, Ronaldo alifunga vyema baada ya kumiminiwa majalo na Dani Carvajal, akatengeneza la pili baada ya Schalke kukosa bao kwa shuti la Felix Platte kugonga mwamba.

Schalke wanaofundishwa na mchezaji na kocha wa zamani wa Chelsea, Roberto Di Matteo walimpoteza mchezaji wao hatari, Klaas-Jan Huntelaar aliyeumia kabla ya mapumziko, na kuwa pigo kubwa kwao.
Katika mechi nyingine, FC Basel na FC Porto wamekwenda sare ya 1-1.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version