Menu
in , ,

Harry Kane ajituliza Bayern

Tanzania Sports

MSHAMBULIAJI Harry Kane amejituliza Bayern Munich licha ya wazo lake la awali la kutana kurejea kwenye Ligi Kuu ya Rngland (EPL) na sasa anasubiri kupata mkataba mpya hapo Bayern.

Kane amesema kwamba matamanio yake ya kurudi Uingereza yametulia na sasa anataka aendelee kuwatumikia waajiri wake wa sasa. Alikuwa mshambuliaji nyota wa Tottenham Hotspur kabla ya kutimkia Ujerumani.

Mchezaji huyo amekamilisha nusu ya mkataba wake wa miaka minne aliosaini 2023 msimu wa kiangazi gharamna yake ikiwa ni pauni milioni 86.kwa sasa ana umri wa miaka 32, akiwa amefunga mabao 103 katika mechi 106 alizocheza katika klabu hiyo kubwa ya Ujerumani. Alisaidia klabu yake kutwaa Kombe la Bundesliga msimu wa 2024/5.

Nahodha huyo wa England anasema kwamba kwa sasa hana tena hamu ya kurudi kuchezea England, tofauti na ilivyokuwa kipindi kifupi kilichopita, bali anachofikiria sasa ni kuongeza kandarasi hapo hapo Bayern.

“Kwa upande wa kubakia hapa muda mrefu zaidi, ni wazi kwamba naliona hilo. Nilizungumza wazi hili wiki kadhaa zilizopita. Hatujadili tena mambo hayo na Bayern ningependa kuzungumza kwa uwazi na uaminifu juu ya hatima yangu hapa.

“Ni wazi kwamba inategemea mwaka kesho na huko mbele na tunafanikiwa lipi Pamoja. Kuhusu Ligi Kuu ya England, sijui. Ungeniuliza kitambo nilipojiunga Bayern, ningekuambia kwamba ningerudi (EPL) lakini sasa naweza kusema Hapana, sitarudi,” akasema Kane.

Kane ni mfungaji bora kwa Spurs na Timu ya Taifa ya England – Three Lions na amekuwa mchezaji aliyefikia idadi ya mabao 100 haraka zaidi . hata hivyo amekuwa mkavu wa vikombe hadi alipokuja kutwaaa akiwa Ujerumani.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version