in ,

Maadui watano wa Simba 2022-23

Kikosi Cha Timu ya Simba Sports Club

MSIMU wa Ligi Kuu Tanzania Bara umemalizika, huku mabingwa wa zamani klabu ya Simba

wakiambulia patupu katika msimu wa pili mfululizo. Simba wamekosa mataji ya Ligi Kuu,

Shirikisho, na Ngao ya Jamii. Kwa hadhi yake, Simba haipaswi kumaliza msimu bila kunyakua

taji lolote. Ingawaje Simba wanayo rekodi ya kunyakua taji la Ligi Kuu mara nne mfululizo

wakiwatimulia vumbi watani wao.

Hata hivyo msimu wa mwaka 2022-23 ni kama ulivyokuwa msimu wa 2021-22, ambako Simba

walipoteza taji lao walilolishikilia misimu minne. Naam, ni namna gani Simba wamepoteza

umwamba katika Ligi Kuu Bara huku wakiwa miongoni mwa wababe wa soka la kimataifa

Afrika? Katika makala haya naangazia maeneo matano makuu ambayo yamedhoofisha ufanisi

wa Simba.

MAWINGA

Ukiangalia orodha ya majina ya wachezaji wa Simba yanatisha sana. Lakini katika idara ya

mawinga imekuwa na wakati mgumu, taarifa toka ndani ya Simba zimebainisha kuwa kocha wa

sasa Robertinho anamhitaji Hassan Dilunga ili awe sehemu ya kikosi cha kikosi chake. Idara ya

mawinga kwa Simba imekuwa changamoto licha ya kuwa na wachezaji kama Pape Ousmane

Sakho, Peter Banda,Kibu Denis kwa kuwataja wachache.

Ni Kibu Dennis pekee ambaye aliibuka katika kikosi cha kwanza cha kocha Robertinho.

Mawinga wa Simba wanatumika kama mbadala wa mbinu, jambo ambalo watani wao wa jadi

wamelitumia kwa msimu mzima kuwategema Jesus Moloko,Farid Mussa na Tusilla Kisinda.

Katika idara hiyo Peter Banda amekwua majeruhi mara kwa mara hali ambayo imekuwa

ikimweka benchi hata pale alipokuwa timamu kiafya. Kifupi Simba wanahitaji kuimarisha eneo

hilo kuwa na mawinga ambao wataleta ufanisi kwa timu yao.

KIUNGO MKABAJI

Kwa msimu mzima Simba wamekuwa wakiwategemea Saido Kanoute na Mzamiru Yassin.

Ikiwa wawili hawa wasipocheza vuziri Simba ilikuwa inapoteana kabisa eneo la katikati. Ujio

wa kiungo mkabajai mwingine Sawadgo hakuwa na tija, ndio maana kocha Robertinho aliamua

kumtupia benchi. Kimsingi Sawadogo hajafikia hata robo ya ufanisi ambao ungeletwa na Jonas

Mkude ambaye msimu huu muda mwingi amekuwa majeruhi pamoja na kushindwa kuonesha

kiwango kizuri.

Kuna baadhi ya mechi Kanoute akiwa majeruhi ilionekana wazi Simba walikuwa wanapata shida

katika mechi kadhaa za Ligi Kuu kwa sababu mategemeo ya injini yao yalikuwa kwa Yassin.

Hilo ni tofauti na watani wao wa jadi ambao wamekuwa na wachezaji watatu wa eneo moja;

Yannick Bangala, Khalid Aucho na Zawadi Mauya. Lakini Simba katika benchi lao kuna

mkongwe Erasto Nyoni, ambaye umri unamtupa mkono. Hili ni eneo ambalo linahitaji

kuimarishwa ili anapokosekana mmoja timu iwe katika uimara uleule.

WASHAMBULIAJI

Kapteni John Bocco ana heshima zake katika Ligi Kuu Tanzania. Majeruhi,kushuka kiwango na

mipango ya mbinu za walimu ni sehemu ya maisha ya wachezaji akiwemo John Bocco. Huyu wa

sasa si Yule aliyetamba misimu kadhaa iliyopita. Si kwamba ameishiwa makali lakini

inaonekana dakika zake kuwepo uwanjani zimepunguzwa na walimu, lakini wabadala wake

hawana uimara kumzidi.

Jean baleke alitoka TP Mazembe kuja kwa mkopo, lakini yeye si mshambuliaji ambaye Simba

wanatakiwa kujivunia au kujaribu kumlinganisha na Chriss Mugalu. Ikiwa uongozi wa Simba

unaweza kufanya maamuzi ya haraka basi Prince Dube wa Azam anaweza kuwa mchezaji wao

muhimu wa kuimarisha eneo la ushambuliaji. Upachikaji wa mabao umepungua sana Simba

kwa sababu ya washambuliaji kutokidhi viwango. Njia pekee ni kusajili washambuliaji wawili

wapya watakaosaidiwa na John Bocco huku Jean Baleke akipewa mkono wa kwaheri.

GOLIKIPA

Ukweli usemwe, nje ya Aishi Manula hakuna golikipa mwenye uwezo wa kukaa langoni mwa

Simba kwa wale waliopo kikosini. Si Ali Salim wala Benno Kakolanya, ni makipa ambao

hawaweza kuvivaa viatu vya Aishi Manula. Matokeo yake Simba kwenye Ligi ya Mabingwa

imefungwa mabao yenye kutia huzuni kama simanzi kwa sababu ya ufanisi hafifu uliopo katika

kikosi chake.

Ikiwa Simba wanataka kuimarisha eneo hilo, ni dhahiri wanatakiwa kutafuta Kipa mwingine

mwenye hadhi angalau ya Metacha Mnacha ambaye licha ya kukaa benchi pale Yanga

unafahamu kabisa ni aina ya golikipa mwenye uwezo mkubwa na uzoefu wa kutosha. Ali Salim

anaweza kusaidiwa kupelekwa mkopo katika timu nyingine ili kuimatishwa uwezo wake. Lakini

litakuwa tukio la uongo kuaminishwa kuwa ndiye mrithi sahihi wa Manula. Vivile Simba

wanahitaji golikipa mwenye uwezo wa kimataifa ambaye anakuwa mbadala wa Manula ili

kuboresha ufanisi wa idara ya makipa ya Simba. Kinyume cha hapo kauli za tumetolewa kiume

zitazidi kila msimu.

MABEKI

Idara hii si mbaya sana, lakini inaleta swali itakuwaje siku Hennock Inonga akichoka? Je

waliopo benchi wanakidhi vigezo vya kuchukua nafasi zao? Inonga ndiye beki ambaye amekuwa

akicheza kwa ufanisi mkubwa Simba. Lakini yeye si roboti kwa maana hiyo nahitaji mabeki

mbadala ambao wanaweza kumpumzisha wakati timu ikiendelea na mipango ya mechi nyingine.

Lakini hali iliyopo Simba iwapo Inonga akipata majeruhi inaonekana wazi wabadala wake

hawafiki hata nusu ya kiwango na ubora alionao Mkongamani huyo. Nini Simba wanachoweza

kufanya? Ni rahisi kwakuwa ni timu inayotikisa mara kwa mara soka la Afrika ni wazi itakuwa

inawavutia wachezaji wengi kupitia timu kwa maana ya kuonekana kimataifa. Ni jukumu la

Simba wenyewe kuimarisha eneo hili. Mabeki wa kuchezea Simba wawe na viwango na ubora

wa hali ya juu. Simba imefika hadhi ya kuwashawishi wachezaji kutoka vilabu mbalimbali hapa

Afrika. Naamini wapo mabeki ambao wanaweza kuisaidia zaidi kwa mbinu tofauti kulingana na

mechi.

USHINDANI LIGI KUU

Mwisho kabisa niwaambie mashabiki wa Simba, adui wa nyongeza ni ushindani. Ligi yetu

imekua na imepata wachezaji wazuri waliopo katika timu zingine. Kwahiyo ushindani kati ya

timu za Ligi Kuu umekuwa mkubwa hali ambayo inazifanya timu kongwe na kubwa kukutana na

wakati mgumu. Njia pekee ya kushinda katika hilo ni kusajili wachezaji wazuri zaidi yao na

kuweka malengo ya kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa. Kwa sasa Simba haiapswi

kumwambia mwalimu eti malengo ni robo fainali badala yake iwe fainali na akishindwa

anaruhusiwa kuondoka pasipo malipo yoyote ya fidia kwa vile atakuwa hajafikisha

walichokubaliana.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

72 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0
Tanzania Sports

Madhila ya Chelsea, Spurs yafute ukocha wa muda

Tanzania Sports

Dakika za lala salama kuwapasua vigogo EPL