in , , ,

Chelsea nusu fainali Europa

*Spurs, Newcastle watolewa

 

Chelsea wamefanikiwa kufika nusu fainali ya Ligi ya Europa, huku Tottenham Hotspurs na Newcastle wakitupwa nje.
Chelsea walijihakikishia nafasi kwenye nusu fainali licha ya kucheza hovyo kipindi cha pili Alhamisi hii kwenye mechi ya marudiano dhidi ya Rubin Kazan nchini Urusi.
Waliingia kwa kiburi cha ushindi wa mabao 3-1 katika mechi ya awali, kisha wakapata bao la dakika ya tano la Fernando Torres na kudhani walishavuka.
Hata hivyo, Ivan Marcano alisawazisha kwa kichwa dakika ya 51 kabla ya Victor Moses kutupia la pili dakika nne tu baadaye.
Kazan waliongeza mabao mawili kupitia kwa kiki ya Gokdeniz Karadeniz na penati ya Bebras Natcho dakika ya 62 na 75, ambapo walihitaji bao moja zaidi, ambalo hawakupata hata hivyo.
Spurs kwa upande wao walipoteza mechi kwa mikwaju ya penati, baada ya kutoka sare ya 2-2 dhidi ya Basel ya Uswisi, matokeo sawa na yalivyokua White Hart Lane mechi iliyopita.
Tom Huddlestone na Emmanuel Adebayor walikosa penati zao wakati Basel wakizifunga kiufundi bila wasiwasi na kuwarejesha nyumbani waendelee kupambana kutafuta nafasi ya nne ili wacheze Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Magoli ya Spurs katika muda wa kawaida yalifungwa na Mmarekani Clint Dempsey, wakati yale ya wenyeji yalifungwa na Mohamed Salah na Aleksander Dragovic.

20130401-225647.jpg

Spurs walimaliza wakiwa 10, kwani beki wao, Jan Vertonghen alipewa kadi nyekundu kwa mchezo wa rafu.
Wawakilishi wengine wa England, Newcastle walitupwa nje ya michuano hiyo na Benfica ya Ureno, baada ya kushindwa kutumia vyema uwanja wa nyumbani.
Newcastle walikuwa na deni la 3-1 waliyofungwa mechi ya kwanza, na Alhamisi hii wanaweza kuwalaumu waamuzi, kwani mabao mawili ya Papiss Cisse yalikataliwa, likaja kukubaliwa moja la dakika ya 71.
Wakati wakitafuta bao la pili ili kuweka mambo sare, muda uliwatupa mkono na dakika ya 90 Benfica walifunga kupitia kwa Eduardo Salvio.
Katika mechi nyingine, Lazio walitoka sare ya 1-1 na Fenerbahce. Kwa matokeo ya robo fainali hiyo ya pili, timu zilizovuka ni Basel, Benfica, Chelsea na Fenerbahce.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Messi aokoa jahazi Barcelona

UJUMBE WA FIFA KUWASILI TANZANIA APRILI 15, 2013