in

Waziri Mkuu Kufungua Mashindano ya Netiboli

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda atakuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mashindano ya taifa ya netiboli yatakayofanyika kuanzia Juni 29 hadi Julai 2 kwenye Uwanja wa Ndani wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Katibu mkuu wa Chama cha Netiboli (Chaneta), Mwajuma Kisengo alisema hadi sasa ni mikoa 13 tu ndio imethibisha kushiriki mashindano hayo.

”Maandalizi yote yamekamilika,” alisema.”Tunatarajia Waziri Mkuu Mizengo Pinda ndiye atakayetufungulia mashindano haya. Natoa wito kwa wakazi wa Dar es Salaam kufika kwa wingi kushuhudia mashindano haya.”

Awali walipanga tarehe ya mwisho ya kuthibisha kushiriki wa mashindano hayo kuwa ni Juni 15 lakini waliamua kusogeza mbele hadi leo ili baadhi ya mikoa iliyokuwa haina uhakika wa kupata fedha kwa ajili ya kufanikisha ushiriki wake.

Alisema baada ya tarehe ya mwisho ya kuthibisha kushiriki ambayo ni leo, mikoa ambayo itakuwa haijathibitisha itakuwa imejitoa katika mashindano ya mwaka huu na kwamba siku mbili baadaye ratiba nzima ya mashindano hayo itapangwa.

Aliitaja mikoa iliyothibitisha kuwa ni Dar es Salaam, Iringa, Kilimanjaro, Tanga, Dodoma, Mwanza, Lindi, Mbeya, Manyara, Kagera, Morogoro na Pwani.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Soka ya Tanzania na kina Eto’o wao

TAVA organises volleyball course for juniors