Menu
in , , ,

Ratiba Ligi Kuu England yatolewa 2015/16

Kipa wa Chelsea, Petr Cech (33) amewapa matumaini mapya Arsenal baada ya kusema kwamba angependa kubaki London.

*Chelsea wanaanzia nyumbani

Msimu mpya wa Ligi Kuu ya England (EPL) utaanza wiki mja mapema kuliko mwaka jana. Utaanza wiki moja na Football League.

Ratiba ya Ligi Kuu ya England imetoka, ambapo mabingwa Chelsea, wanaanza kutetea ubingwa wao kwa kuwakaribisha Swansea.

Hiyo itakuwa wikiendi ya Agosti 8 na 9 mwaka huu, msimu mpya utakapoanza wakati Manchester City waliomaliza pointi nane nyuma ya Chelsea watasafiri hadi kwa West Bromwich Albion.

Mechi kumi za mwanzo wa msimu 2015/16-EPL
Mechi kumi za mwanzo wa msimu 2015/16-EPL

Arsenal waliomaliza katika nafasi ya tatu wataanza na West Ham wakati waliokuwa wa nne, Manchester United watakabiliana na Tottenham Hotspur katika dimba la Old Trafford.

Liverpool wasiojulikana kama bado watakuwa na Raheem Sterling watapepetana na Stoke, huku Newcastle wakitoana jasho na Southampton wakati Leicester watawakaribisha Sunderland.

Vijana waliopanda daraja msimu huu – Bournemouth, Watford na Norwich watakabiliana na Aston Villa, Everton na Crystal Palace kwa mtiririko huo.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Exit mobile version