in , , , ,

Mourinho amtishia Hazard

*Guardiola hajui hatima yake

Matokeo mabaya kwenye nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL) yamewachanganya makocha wa Chelsea na Bayern Munich.

Wakati Jose Mourinho wa Chelsea akimalizia hasira zake kwa mchezaji kinda na mahiri, Eden Hazard kwa kumchagiza, Pep Guardiola amesema kwamba Bayern wanatakiwa kutafakari iwapo yeye ndiye anafaa kuwa kocha wao.

Hazard alimbwatukia kocha wake kwa mbinu zake na sasa Mourinho amemtishia huku akisema kwamba winga huyo bado hajaanza kujituma kabisa kwa ajili ya klabu yake.

Inaelezwa kwamba Paris Saint-Germain wa Ufaransa wanamwania Hazard kwa ajili ya msimu ujao na ndiye amekuwa nguzo muhimu kwa Chelsea lakini timu hiyo ya London ilifungwa 3-1 na Atletico Madrid Uwanja wa Stamford Bridge na kuwachukiza washabiki wa Chelsea.

Mourinho anasema kwamba Hazard alifanya makosa kwenye mechi hiyo na kuruhusu bao la kwanza na kusema ni aina ya wachezajiw asiotoa suluhu ya tatizo bali wanalaumu tu.

Katika hatua nyingine, Guardiola amesema kwamba ni juu ya Bayern kuamua hatima yake. Bayern walifungwa 4-0 na Real Madrid.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Ubingwa Ulaya waenda Hispania

Man City washindwe wenyewe