in , , ,

Manchester United Ngao ya Jamii

Mabingwa watetezi wa England, Manchester United wamempa kocha mpya, David Moyes zawadi kwa kutwaa Ngao ya Jamii.

Katika mechi iliyokipigwa katika Uwanja wa Wembley dhidi ya klabu inayoshushwa daraja msimu uliopita ya Wigan, Mdachi Robin van Persie alipachika mabao mawili na kumwondolea shaka kocha huyo Mskochi.

Moyes amekuwa katika majadiliano juu ya hatima ya Wayne Rooney, mchezaji aliyemzindua akiwa Everton kisha akaja kumkuta Man U, lakini ameshaomba zaidi ya mara moja kuondoka.

Ushindi huo umekuwa liwazo Old Trafford, kwa vile katika mechi ya kwanza ya Moyes hapo, walifungwa mabao 3-1 na Sevilla ya Hispania majuzi.

Moyes ameweka wazi kwamba chaguo lake la kwanza kwa mshambuliaji wa kati ni RVP na kwamba Rooney anaweza kusota benchi, lakini Mwingereza huyo anadhani muda aliokaa hapo unatosha.

Iliwachukua Man U dakika sita tu kupata bao la kwanza na baada ya hapo Wigan wanaofundishwa na Owen Coyle waligangamala. Hata hivyo dakika ya 59 ilikuwa tena chungu kwao, kwani Mdachi huyo aliyehamia United kutoka Arsenal msimu uliopita, alipachika bao la pili.

Enhanced by Zemanta

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

MAKOCHA 32 KUSHIRIKI KOZI YA FIFA COPA COCA-COLA

Tunahitaji Kumbukumbu Sahihi za miaka ya nyuma kwenye soka…