in , , ,

Man City safi, Liverpool waamka

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu England (EPL), Manchester City wamepata ushindi wa 2-0 dhidi ya Aston Villa, lakini baada ya kubanwa hadi dakika ya 81 ya mchezo.

Villa walioanza ligi vyema kabla ya kufungwa mfululizo, walicheza vizuri na mechi ilikuwa na kila aina ya ushindani, ndipo Yaya Toure alipofanikiwa kuzifumania nyavu dakika ya 82 kwa guu la kushoto baada ya kupata pasi ya Fernando.

Sergio Aguero alimaliza kazi dakika sita baadaye alipopata pasi ya James Milner na kuwapeleka City hadi nafasi ya pili ya msimamo wa ligi japokuwa kubaki hapo itategemea matokeo ya mechi nyingine leo.

Liverpool waliokuwa doro kwenye mechi zilizopita walipata ushindi muhimu dhidi ya West Bromwich Albion, kupitia kwa mabao ya Adam Lallana na Jordan Henderson, huku Saido Beraniho kutoka Burundi akiwafungia West Brom kwa mkwaju wa penati.

Katika mechi nyingine, Sunderland waliwafunga Stoke 3-1, Swansea wakatoshana nguvu ya mabao 2-2 na Newcastle, Hull wakawapiga Crystal Palace 2-0 wakati Leicester na Burnley walitoka pia sare ya 2-2.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Weusi wabaguliwa ukocha England

Chelsea hawakamatiki