Menu
in , , , ,

Mambo yaanza Guinea

*Wenyeji sare, Gabon wawafyatua Burkina Faso

Wenyeji wa michuano ya 30 ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), Guinea ya Ikweta nusura waanze kwa ushindi, baada ya kuwa mbele kwa bao moja hadi dakika tatu kabla ya mechi kumalizika, Kongo Brazzaville waliposawazisha.

Guinea wanaochukuliwa kuwa si wazuri, walipata bao kupitia kwa mchezaji wa Middlesbrough ya England, Emilio Nsue dakika ya 16 tu, na walililinda vyema hadi dakika za mwisho mwisho walipozidiwa.

Kwenye mechi iliyopigwa katika Uwanja wa Bata, washabiki walianza kufurahia ushindi lakini Kongo walijizatiti kipindi cha pili kwa mashambulizi mfululizo, ambapo mpira wa Francis N’Ganga uligonga mwambakabla ya mshambuliaji wa West Bromwich Albion, Thievy Bifouma kusawazisha dakika ya 87.

Ilikuwa mechi ya fungua dimba iliyoanza vyema, licha ya kuwapo na wasiwasi kutoka kwa baadhi ya watu juu ya utayari wa taifa hilo dogo kuandaa mashindano hayo peke yake na kwa notisi ya muda mfupi. Mwaka 2012 walikuwa wenyeji wenza na Gabon.

Taifa hilo, ambalo timu yake inajulikana kwa jina la National Thunder (Radi ya Taifa) liliandaa michuano hii kutokana na Morocco waliokuwa waandae kutaka isogezwe mbele kwa hofu ya maradhi ya Ebola yaliyozikumba nchi za Liberia na Sierra Leone, kisha wakajitoa.

Katika mechi nyingine, Gabon waliwapiga Burkina Faso kwa mabao 2-0. Burkina Faso walikuwa washindi wa pili kwenye michuano ya mwaka jana. Mabao ya washindi yalifungwa na mshambuliaji wa Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang na Malick Evouna.

Burkina Faso walikuwa na mchezo mzuri, hata hivyo, huku mshambuliaji wa Chelsea aliye kwa mkopo Vitesse Arnhem, Bertrand Traore akionesha makali yake, lakini kipa wa Gabon, Didier Ovono alikuwa kizingiti kikubwa kwake.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version