in , , ,

Ghana, Ivory Coast nusu fainali AFCON

Ghana na Ivory Coast wamefanikiwa kuingua nusu fainali michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCPN) kwa kuwafunga kirahisi Guinea Bissau 3-0.

Kwa Ghana Christian Atsu alilianzisha dakika nne tu za kwanza, baada ya kufunga kutokana na mpira aliofinyiwa kwa nyuma na from Andre Ayew. Guinea waliwazawadia Ghana bao la pili baada ya Baissama Sankoh kushindwa kusafisha mpira na Kwesi Appiah bila ajizi akaukwamisha kimiani.

Alikuwa ni Atsu tena aliyecheka na nyavu na kuwafanya Black Stars hao watoke na ushindi mnono, tofauti na timu nyingine ambazo tangu mwanzo ushindi umepatikana kwa mbinde.
Katika mechi nyingine, Ivory Coast walifanikiwa kuwatoa Algeria waliokuwa wakipewa nafasi ya kufanya vyema kwenye mashindano haya, tena wakatoka kwa kukandamiziwa mabao 3-1.

Mshambuliaji mpya wa Manchester City, Wilfried Bony aliwaonesha kile watakachokuwa wakipata kutoka kwake, kwa kupachika mabao mawili, huku Gervinho akifunga jingine na kuwahakikishia Tembo wa Afrika kusonga mbele.

Hata hivyo, ushindi haukuja kirahisi wala mapema, kwani bao la kwanza la Bony lililopatikana dakika ya 26 lilisawazishwa na Hilal Soudani katika dakika ya 51. Awali mchezaji huyo alikaribia kufunga lakini jitihada zake zikakwama kwa kipa Sylvain Gbohouo.

Algeria walitia shinikizo kwenye lango la Ivory Coast katika dakika za mwisho, lakini hawakuweza kufanikiwa kupata bao hadi kipenga cha mwisho.
Nusu fainali ya kwanza ni baina ya Kongo Kinshasa na Ivory Coast Jumatano hii wakati ya pili ni kati ya Ghana na wenyeji Guinea ya Ikweta waliovuka kiaina. Mshindi wa tatu atatafutwa Jumamosi wakati fainali ni Jumapili.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Arsenal heshima imerudi mjini

KAGERA SUGAR KUHAMA UWANJA