in

Kombe la Mpira wa Kikapu kufanyika Oktoba Dar

MASHINDANO ya mpira wa kikapu ya Kombe la Taifa yatafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Oktoba 19 hadi 25, kwa mujibu wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania, TBF.

Katibu Mkuu wa TBF, Lawrence Cheyo alisema mashindano hayo yatafanyika baada ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

“Tumeona tufanye mashindano haya baada ya mwezi mtukufu wa ramadhani ili tuyafanye kwa uhuru zaidi na wachezaji wakiwa na nguvu,” alisema

Alisema mashindano hayo yatashirikisha mikoa yote ya Tanzania Bara.

”Mikoa ianze kujiandaa mapema kuanzia nauli ya kuja katika mashindano na ya kurudi, pia kila timu iwe na wachezaji wasiozidi 12, tunatarajia mikoa husika itazisaidia timu fedha kwa ajili ya mashindano.”

”Tunataka mashindano ya mwaka huu yawe na msisimko hivyo timu zijitahidi kufanya mazoezi ya nguvu kuhakikisha zinafanya vizuri,” alisema

Alisema mwisho wa mikoa kuthibitisha ushiriki wao ni Agosti 30 na iwapo timu haitathibitisha ifikapo wakati ule itaondolewa mashindanoni. Bingwa mtetezi wa michuano hiyo ni Mkoa wa Dar es Salaam kwa wanaume na wanawake.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Ziara ya Real Madrid Tanzania yaibuka upya Bungeni

Premier League – Villa: Barry transfer saga over