Menu
in , , ,

Hakuna haja ya “kupaniki” Van Dijk kwa Liverpool

• Nahodha wa Liverpool anakiri “tunahitaji kuboresha”
• Slot asema Alisson ana uwezekano wa 99.9% wa kukosa safari ya Chelsea


Virgil van Dijk amesisitiza kwamba Liverpool haipaswi kuwa na hofu licha ya kupoteza mechi mbili mfululizo kwa mara ya pili tu chini ya Arne Slot, kufuatia kipigo dhidi ya Galatasaray. Maumivu ya majeraha kwa Alisson na Hugo Ekitiké yameongeza wasiwasi kwa Liverpool, huku kocha wao mkuu akitetea kiwango cha timu na uamuzi wake wa kumpumzisha Mohamed Salah huko Istanbul.

Mkwaju wa penalti wa kipindi cha kwanza uliopigwa na Victor Osimhen uliihakikishia Galatasaray ushindi katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Viongozi wa Ligi Kuu ya England walikuwa tayari wamepoteza rekodi yao ya ushindi wa 100% msimu huu baada ya kufungwa na Crystal Palace Jumamosi, lakini Van Dijk alisisitiza kuwa kikosi kilichofanyiwa mabadiliko kitaweza kurejea kwenye kiwango cha kushindania ubingwa.

Tanzania Sports
Matokeo mengine UEFA

Nahodha huyo wa Liverpool alisema:
“Naamini tumeonyesha uwezo wetu tayari kwenye mechi nyingi msimu huu, lakini bado hatujaweza kufanya hivyo kwa dakika zote 90, jambo ambalo kwa bahati mbaya ni kweli. Hili ni jambo la kawaida kabisa, na siku hizi huna muda wa kusubiri huruma ya dunia ya nje, kwa hiyo tunatakiwa kuwa na nguvu kiakili.
“Nina imani kubwa. Tunapaswa kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kushikamana. Tumeanza msimu vizuri kwa upande wa pointi. Hakuna haja ya hofu, lakini tunapaswa kuboresha.”

Slot alithibitisha kwamba kipa Alisson atakosa safari ya kwenda Stamford Bridge kucheza na Chelsea Jumamosi kutokana na tatizo la misuli. Ekitiké naye aliondolewa uwanjani kipindi cha pili kutokana na jeraha lisiloelezwa wazi, baada ya kushika sehemu ya nyuma ya mguu wake mwishoni mwa mchezo.

“Alisson alihisi kitu alipokuwa akikimbia kurudi nyuma,” Slot alisema. “Kwa kawaida, mchezaji akikimbia haraka kisha anahisi maumivu, anaanguka chini na harudi tena uwanjani — na kumbuka, wachezaji hufanya hivyo mara nyingi, wanarudi uwanjani baada ya dakika chache bila maumivu — basi huwa nahofia jambo baya, na ndivyo ilivyotokea kwa Alisson. Hatacheza Jumamosi, uwezekano ni 99.9%.”

Kuhusu kipigo cha hivi karibuni cha Liverpool, kocha huyo mkuu alisema:
“Kwangu mimi hiki kilikuwa kipigo tofauti na kile dhidi ya Palace, kwa sababu kulikuwa na mambo mengi mazuri, hasa katika kipindi cha kwanza.
“Kipindi cha pili kilikuwa kigumu zaidi kwa sababu kwanza kabisa wapinzani walipambana kwa nguvu zote, jambo ambalo wanastahili pongezi, na pili mpira haukuwa uwanjani mara nyingi katika kipindi cha pili.”

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version