in , , ,

Chelsea watandikwa 3-0

*Fabregas alambwa kadi nyekundu

West Bromwich Albion wametibua mwendelezo wa sherehe za ubingwa wa Chelsea kwa kuwatandika mabao 3-0.

Katika hali ya kushangaza, kocha Jose Mourinho amelalamikia klabu nyingine kwa kichapo hicho, akidai hazikuonesha ushindani wa kutosha kwenye Ligi Kuu.

Aliyeanza kupeleka kilio kwa The Blues alikuwa ni mzaliwa wa Burundi, Saido Berahino ambaye pia alifunga la pili kwa penati kabla ya Chris Brunt kutia la tatu.

Penati hiyo ilitolewa baada ya nahodha wa Chelsea, John Terry kumwangusha Beraniho ndani ya eneo la penati.

Chelsea walimaliza mechi wakiwa 10 baada ya kiungo wake wa kimataifa wa Hispania, Cesc Fabregas kupewa kadi nyekundu.

Fabregas alipewa kadi nyekundu kwa kitendo chake cha kumpiga kwa mpira Brunt. Hiki kilikuwa kipigo cha tatu kwa Chelsea kwenye ligi msimu huu.

Kabla ya mechi hii Chelsea walikuwa wamekwenda michezo 16 bila kufungwa. Mshambuliaji wa kati wa Chelsea, Diego Costa naye alionekana kukwaruzana na beki wa kati wa West Brom, Gareth McAuley kiasi cha mwamuzi Mike Jones kuingilia kati kuwapatanisha.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Yanga, Simba mbio za usajili

Sterling hawataki Liverpool