in , , ,

Chelsea waoga kichapo cha kwanza

Yametimia! Ndivyo unavyoweza kusema kwa vinara wa Ligi Kuu ya England, Chelsea kuambulia kichapo cha kwanza msimu huu.
Vijana wa Jose Mourinho walijizatiti kwa kushinda na mara chache kutika sare, lakini kwa gwaride la wachezaji wa Newcastle, wameishia kuwa mbendembende na ni leo baadhi ya wachezaji hao wamejua kufungwa Chelsea kunaumaje.

Newcastle wakicheza nyumbani na kwa kujiamini licha ya kuanza ligi kwa kusuasua msimu huu, walimaliza wakiwa wachezaji 10, kwani Steven Taylor alipewa kadi ya pili ya njano, na hivyo nyekundu kwa kumchezea vibaya André Schürrle katika dakika ya 80.

Mabao ya Newcastle yalitiwa kimiani na mchezaji aliyetamba misimu miwili iliyopita kabla ya kuwa doro, Papiss Cisse dakika za 57 na 78 wakati la kufutia machozi la Chelsea lilifungwa na Didier Drogba dakika ya 83.

Mourinho alisema kabla ya mechi hiyo kwamba alitarajia Newcastle wanaofunzwa na Alan Pardew wacheze gemu kali wanayokuwa nayo nyakati Fulani Fulani.

Kadhalika kichapo hicho kinakuja siku moja tu baada ya Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger kutamka kwamba Chelsea wanakamatika. Hadi kabla ya mechi hiyo walikuwa wanaongoza kwa pengo la pointi sita, wa pili wakiwa Manchester City.

Katika mechi hiyo, kipa wa Newcastle, Rob Elliot aliumia na nafasi yake kuchukuliwa na kinda la miaka 21, Jak Alnwick. Hii ilikuwa mechi ya 15 msimu huu kwa Chelsea na Newcastle kwenye ligi kuu.

Cisse alifunga bao la kwanza baada ya beki Garry Cahil kushindwa kuzuia majalo iliyokuwa aimeingizwa kwenye eneo lao na Sammy Ameobi. Shuti la Eden Hazard baadaye lilimfikia Moussa Sissoko aliyekianzisha tena akampatia Cisse na kumfunga kipa Thibaut Courtois aliyekuwa hajafungwa kwenye ligi hii.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Chelsea, Man City, Arsenal waua

Balotelli matatani tena