Menu
in , , ,

Chelsea, Liverpool nusu fainali

Chelsea na Liverpool wamepangwa kuchuana kwenye nusu fainali ya Kombe la Ligi, maarufu zaidi kaa Capital One Cup.
Chelsea wanaoongoza Ligi Kuu ya England wamepata nafasi hiyo baada ya kuwachakaza Derby 3-1 wakati Liverpool waliwafunga Bornemouth 3-1 usiku wa Jumatano hii, mabao mawili yakifungwa na Raheem Sterling aliyekuwa na ukame wa mabao wa muda mrefu. Jingine lilifungwa na Lazar Markovic.

Katika nusu fainali nyingine ya kombe hili dogo, Tottenham watacheza na Sheffield United, baada ya vijana hao wa Mauricio Pochetino kufanikiwa kuwafunga Newcastle 4-0 na kuwaongezea uchungu, kwani kwenye mechi ya ligi kuu iliyopita, Arsenal waliwachakaza kwa 4-1.

Sheffield United si wa kuchezea, kwani kwenye michuano kama hii walipata kuwafunga na kuwatupa nje Southampton na West Ham. Zitakuwa mechi mbili kwa kila timu na zitachezwa mwezi ujao, huku fainali ikiwa Machi mosi mwakani.

Kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers amefurahia matokeo hayo, ikizingatiwa kwamba hawafanyi vyema kwenye ligi kuu na amesema kwamba atajitahidi walau akapate kikombe hicho kama faraja, kwani pia wametupwa nje ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Ni majuzi tu walifungwa 3-0 na Manchester United kwenye ligi kuu ya England na wanakabiliana na Arsenal wikiendi hii katika michuano hiyo hiyo. Amekuwa kwenye shinikizo la timu kufanya vyema, na inadaiwa Wamarekani wanaoimiliki Liverpool wanafikiria kumfukuza iwapo timu itaendelea kufanya vibaya.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version