Menu
in , ,

Arsenal wawakung’uta Bayern

 
Arsenal wamefufua matumaini yao kwenye hatua ya makundi katika Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL) baadaya kuwafunga Bayern Munich 2-0.

Wakicheza mbele ya maelfu ya washabiki wao katika dimba la Emirates Jumanne usiku, Washika Bunduki wa London walipata mabao yao kupitia kwa mshambuliaji wa kati, Olivier Giroud na kiungo Mesut Ozil.

Kocha Arsene Wenger alitangulia kusema kabla ya mchezo kwamba Bayern walikuwa na udhaifu kwenye baadhi ya maeneo, huku matumaini ya washabiki yakiwa yamepotea baada ya kukubali vichapo viwili kwenye mechi za mwanzo.

Haikuwa kazi rahisi, hata hivyo, kuwashinda Wajerumani hao wanaofundishwa na Pep Guardiola, na ilibidi Arsenal wasubiri hadi dakika ya 77 kupata bao la kuongoza lililotiwa kimiani na Giroud, baada ya kipa Manuel Neur kufanyia kosa mpira wa adhabu ndogo wa Santi Cazorla.

Advertisement
Advertisement

Bayern walitawala mpira kwa ujumla, lakini Arsenal walitumia mbinu kuhakikisha wanashinda, ambapo bao la pili lilifungwa na Ozil akiitendea haki majalo ya beki wa kulia, Hector Bellerin ambaye sasa amekuwa mzuri katika kupandisha mashambulizi.

Neur alijaribu tena kuuondoa mpira huo lakini waamuzi wakamaizi kwamba ulishavuka mstari mweupe na kuwa bao la pili lililoshangiliwa hasa na Arsenal. Kipa Petr Cech wa Arsenal alifanya kazi ya ziada, akiziba makosa yaliyofanywa awali na David Ospina kwenye mechi dhidi ya Olympiakos.

Arsenal walitakata hapo jana

Aliokoa hatari mbili kubwa zaidi kutoka kwa Thiago Alcantara na Arturo Vidal. Arsenal bado wana kazi kubwa ya kufanya kwenye mechi za marudiano, kwani wanashika nafasi ya nne wakiwa na pointi tatu sawa na Dinamo Zagreb, wakati Olympiakos wanazo sita sawa na Bayern Munich.

Katika matokeo mengine, BATE Bor walifungwa 2-0 na Barcelona, Bayern Leverkusen wakaenda sare ya 4-4 na Roma, Dynamo Kiev wakaenda suluhu na Chelsea, Fc Porto wakawafunga Maccabi Tel Aviv 2-0, Valencia wakashinda 2-1 dhidi ya KAA Gent na Zenit St Petersburg wakawafunga Lyon 3-1

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Exit mobile version