Menu
in , , ,

Yanga wawasha moto

Leo ilikuwa kama unamsukuma mlevi, ambapo mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Tanzania , Yanga, waliwakandamiza JKT Ruvu kwa mabao 5-1.

Wakicheza tena na kipa wao namba moja, Deogratius Munish baada ya Juma Kaseja kucheza mechi ambazo Dida alikuwa ameumia.

Walikuwa na wakati mzuri tangu mechi kuanza, ambapo kama kuna siku Mrisho Ngasa alicheza vyema ni Jumapili hii, ambapo alifunga hat-trick pia Munishi alikuwa mzuri mno langoni.

Mabao mengine yalifungwa na Didier Kavumbagu na Hussein Javu katika mechi ambayo Yanga walicheza kwa kujidai na kujimegea nafasi nyingi za kuatisha vijana wa kocha wao msaidizi wa zamani, Freddy Felix Kataraiya Majeshi Minziro aliyefarijiwa na bao la Nashon Naftali dakika saba kabla ya mpira kumalizika.

Yanga sasa watajiuliza kwa mechi zijazo, kwa sababu wamefikisha pointi 49 wakati Azam wanazo 53 wakiwa wamecheza mechi sawa. Mbeya City wana pointi 46 wakishika nafasi ya tatu.

Yanga wanatakiwa kuwaombea Azam matatizo kwenye mechi zilizobaki, nao washinde, au pia wafanikiwe kwenye rufaa yao dhidi ya Mgambo JKT.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version