in

Thadeo: Hali ya michezo Nchini hairidhishi…

MKURUGENZI wa Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Leornad Thadeo amesema mwenendo na hali ya michezo nchini bado hauridhishi kwa sasa kutokana na nchi kushindwa kufanya vizuri katika michezo kimataifa.

Hata hivyo, mkurugenzi huyo alikimwagia sifa chama cha netiboli nchini kwamba ni mfano kuigwa kwa kuwa kimefanikiwa kutumia jitihada zake kuinua mchezo huo nchini.

Akihojiwa katika kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na kituo cha luninga ya serikali cha TBC, Thadeo alikiri kwamba mwamko wa michezo nchini bado uko chini kutokana na kukabiliwa na changamoto mbalimbali.

“Mwenendo wa michezo nchini siyo mzuri sana, kwani bado hatujafanya vizuri katika mashindano ya kimataifa, mwenendo sio mzuri kwa sasa, “alisema Thadeo.

Thadeo alisema baadhi ya vyama vya michezo nchini vimekuwa vikiongozwa bila kufuata katiba ya vyama huku akidai vingine vimejikita kwenye migogoro badala ya kukazania maendeleo ya michezo hali inayosababisha michezo nchini kushindwa kufanya vizuri kimataifa.

Alisema serikali imeandaa mpango mkakati wa michezo nchini ambao utakamilika mwezi ujao ambao utalenga kuleta maendeleo ya michezo nchini sanjari na kuonyesha dira kwa vyama mbalimbali vya michezo nchini.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

UMISETA games wind up

Defending champions Spain claimed an historic third successive major trophy with a 4-0 rout of Italy in the Euro 2012 final in Kiev Sunday.