in

TFF yataka makatibu ndani ya vilabu vya ligi kuu-Mwakalabela

Shirikisho la soka nchini TFF limevitaka vilabu vya soka vya ligi kuu Tanzania bara kuharakisha mchakato wa kupata viongozi watendaji wa vilabu vyao kabla ya msimu wa mpya wa ligi kuu Tanzania bara haujaanza mwezi ujao.

Nafasi ambazo zinatakiwa kuwa na viongozi watendaji  wa kuajiliwa ni pamoja na Katibu mkuu, Msemaji na Mweka Hazina wa klabu.

Katibu mkuu wa TFF Fredrick Mwakalebela amesema hilo ni azimio la mwaka 2007 lililofanyika mjini Bagamoyo mkoani Pwani baina ya viongozi wa vilabu hivyo na TFF  ambapo vilabu hivyo vilikubaliana kuwa na viongozi hao, huku azimio la mwaka 2010 likiwa ni la kuboresha miundombinu ya vilabu ikiwa ni pamoja na ujenzi wa viwanja vya klabu.

TFF imesema hadi sasa hakuna timu hata mmoja ya ligi kuu  iliyopeleka jina la mtendeji wake wa kuajiliwa na TFF inasema bila kufanya timu husika hatoruhusiwa kushiriki ligi kuu msimu ujao.

TFF ilikutana na viongozi wa timu hizo za ligi kuu hapoa jana Jumanne na mkutano huo utaendelea tena hapo kesho Alhamis kujadili mambo mbalimbali yahusuyo msimu mpya wa ligi hiyo

Wakati huohuo, Shirikisho la soka barani Afrika CAF limetuma barua ya kupendekeza mfumo mpya wa kalenda ya mashindano yake ya  kombe la Shirikisho na lile la  ligi ya Mabingwa barani Afrika, pendekezo ambalo limekubaliwa na TFF.

Katibu huyo wa TFF Mwakalebela amesema TFF imekubaliana na CAF kuhusiana mabadiliko hayo kutokana na kuendana sambamba na kalenda ya TFF inayoanza mwezi July na kukamilika mwezi May kila mwaka husika wa msimu wa soka.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply
  1. Tanzania ili itimie ni mpaka iwepo Tanzania Visiwani yaani Zanzibar nimezipitia habazi zilizo humu zinaizungumzia Tanzania bara tu ningelishauri mkatupitia nasi wa kutoka Zanzibar.

    BY KATIBU MKUU BASKETBALL ZANZIBAR

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

BMT kukutana na TAHA

Cuban coaches land two-year contracts