in

  Tanzania yajaa matumaini kupata medali olimpiki

KIJANA Mtanzania mwenye ulemavu wa miguu,  Zaharan Mwenemti  ni mmoja wa Watanzania watano watakoiwakilisha nchi katika michuano ya Olimpiki itakayofanyika nchini Uingereza mwishoni mwa Julai , mwaka huu.

Mwenemti ambaye kwa sasa anajifua kwa udi atacheza michezo mitatu ambayo ni kurusha tufe, kurusha kisahani na kutupa mkuki.

Mbali ya mchezaji huyo mahiri, pia wapo vijana wapya wane wanaotegemewa kupata medali kwa masuala ya riadha na kuogelea.

Mwenyekiti wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), Filbert Bayi ameviambia vyombo vya habari kwamba ana uhakika vijana wa riadha watatwaa medali  kwenye michuano hiyo itakayotimua vumbi nchini Uingereza.

Matumaini ni makubwa, vijana wanaendelea kujifua vizuri hususan wa riadha’’ alisema alipowazungumzia wanariadha waliopiga kambi katika Mji wa Kibaha kilometa karibu 50 kutoka  Jiji la Dar es Salaam.

Wanariadha tegemeo ni  Samson Ramadhani ambaye anajifua kwa kufukuza upepo katika umbali wa mita 5,000 pamoja na Fustine Mussa na Musendeki Mohamed anayetarajiwa kupata medali ya kuongelea.

Bayi ambaye aling’ara katika riadha mwaka 1980 kwa mbio za mita 3,000 aliwahakikishia waandishi kwamba anayo imani kubwa na wanamichezo wake wanaokwenda kwenye olimpiki.

Kwa upande wa ngumi kijana pekee ni Seleman Kindunda ambaye anajifua usiku na mchana kujiandaa na michuano hiyo.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Basketball Clinic kwa Msaada wa tanzaniasports.com Arusha.

Hotuba ya ufunguzi wa mafunzo ya vijana wa chini ya miaka 17 Arusha tarehe 9, Juni 2012.