in

Pinda ahimiza ushirikiano wa TFF, ZFA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ametaka viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kuandamana na wenzao wa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), ili kudumisha muungano.

Alikuwa akijibu hoja ya Mbunge wa Dimani (CCM), Hafidh Ali Tahiri, aliyedai kuwa TFF inavunja Katiba ya nchi kwa sababu haishirikishi viongozi wa ZFA kwenye ziara zao nje ya nchi.

Pinda alisema sio vibaya viongozi wa TFF kwenye ziara zao nje ya nchi kuandamana na angalau kiongozi mmoja wa ZFA, hali ambayo itaimarisha muungano na kuondoa manung’uniko.

Alisema malalamiko yanayotolewa yana msingi kwa sababu, yanajenga dhana mbaya ya muungano na kuwataka mawaziri kufanya ziara Zanzibar kuangalia maeneo mbalimbali.

Hivi karibuni viongozi wa ZFA walilalamikia kitendo cha viongozi wa TFF kuhudhuria mkutano mkuu wa FIFA katika kisiwa cha Bahamas bila ya kuambatana nao.

Hata hivyo, hivi karibuni maofisa wa TFF walidai kuwa mialiko wanayopata kutoka FIFA huja kwa nyadhifa za viongozi wa TFF, ambao ndio mwanachama wa FIFA.

TFF ndio inayotambuliwa na FIFA wakati ZFA ilikwama maombi yake ya kujiunga na FIFA kutokana na Zanzibar kuwa sehemu ya Jamhuri ya Muungano.

SOURCE: NIPASHE

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Ronaldo agrees six-year Real deal

Tanzania na netiboli