Menu
in , , , ,

Nigeria nje AFCON

Mabingwa watetezi wa Afrika, Nigeria wameshindwa kufuzu kwa michuano ya Klabu Bingwa Afrika (AFCON), hivyo kutema ubingwa rasmi.

Nigeria imeshindwa kufuzu katika kundi ‘A’ ilikokuwa, hivyo itayasikia tu mashindano hayo yaliyopangwa kufanyika nchini Guinea ya Ikweta baada ya Morocco waliokuwa waandae kutofautiana na Shirikisho la Soka la Africa (Caf) juu ya masuala ya Ebola.

Katika mechi ya mwisho iliyofanyika Jumatano hii, Nigeria walibaniwa na Afrika Kusini mjini Uyo, wakaenda sare ya 2-2 hivyo kumaliza michuano nje ya nafasi mbili za juu kwa kundi lao.

Wangeweza kutarajia kupata nafasi ya timu bora zaidi katika nafasi za tatu lakini pia napo wameangukia pua, kwa sababu wana pointi nane tu. Afrika Kusini wamewakata maini Nigeria maana tayari walishafuzu kabla ya mechi hiyo, kwa mashindano yatakayofanyika kuanzia Januari 17 hadi Februari 8 mwakani.

nchi nyingine zilizofuzu kwa mashindano hayo makubwa Afrika ni Algeria, Burkina Faso, Cameroon, Cape Verde, Kongo Brazzaville, Kongo Kinshasa, Guinea ya Ikweta kwa nafasi ya wenyeji, Gabon, Ghana, Guinea, Ivory Coast, Mali, Senegal, Tunisia na Zambia waliofiwa na Rais Michael Satta majuzi.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version