Menu
in , , ,

Mtoto wa Pele jela miaka 33

Wakati Ulimwengu wa Soka ukitazama mbele kwa ajili ya Kombe la Dunia, gwiji wa soka kihistoria, Pele amepata pigo kubwa baada ya mwanawe
Edinho Edson Cholbi do Nascimento kutupwa jela miaka 33.

Edinho (43) ametiwa hatiani kwa makosa ya jinai ya kutakatisha fedha zilizotokana na mauzo ya dawa za kulevya.

Edinho alipata kuchezea Santos akiwa kipa katika klabu ya zamani ya baba yake alikotokea pia Neymar wa Barcelona na baada ya kufikishwa mahakamani alikiri makosa yake hayo.

Aliwahi kukamatwa mwaka 2005 na kutupwa ndani katika operesheni ya kusambaratisha genge la watumiaji, wasafirishaji na wauzaji wa mihadarati katika Jiji la Santos kabla hajaachiwa.

Pele alisema mwaka 2006 kwamba Mungu akipenda haki ingetendeka na kwamba hapakuwa hata tone la ushahidi dhidi ya mwanawe huyo.

Hata hivyo, kwa sasa Edinho atakuwa huru kwa sababua meamua kukata rufaa licha ya kukiri kununua mihadarati anasema hakuwa akifanya kazi na genge hilo hatari.

Mahakama ya Praia Grande ilitoa adhabu kama hiyo kwa washitakiwa wengine watatu na kuamuru mali zao zote zikamatwe na kutaifishwa, zikijumuisha jumla ya magari 100.

Pele ambaye ni Balozi wa Kombe la Dunia na linafanyika nchini mwake, atatakiwa kushughulikia suala la mtoto wake sambamba na mashindano hayo makubwa zaidi ya soka duniani.

Brazil imeshaandamwa kwa kushindwa kukamilisha viwanja kwa wakati, huku baadhi ya wananchi wakiandamana kupinga matumizi makubwa ya fedha kwenye soka wakati hali zao ni mbaya.

Edinho alistaafu soka 1999 wakati baba yake, Pele (73) anachukulia kama moja ya nembo muhimu zaidi za soka duniani.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version