in

Maulid Dilunga hatunaye tena

MCHEZAJI wa zamani wa Yanga na timu Taifa Stars, Maulid Dilunga amefariki dunia juzi usiku kutokana na kusumbuliwa na matatizo ya moyo na ini.

Akizungumza jijini jana, mdogo wa marehemu, Abbas Dilunga ambaye alikuwa akiichezea Simba na Taifa Stars, alisema kaka yake aliugua kwa muda wa miezi mitatu na alilazwa katika Hospitali ya Amana, Muhimbili na baadaye alirudishwa nyumbani hadi mauti ilipomfika juzi.

”Kaka aliugua kwa takriban miezi mitatu na alilazwa katika Hospitali ya Amana, akahamishiwa Muhimbili na kabla ya kurudishwa nyumbani kwake Vingunguti,” alisema Dilunga.

Alisema marehemu huyo aliyejizolea sifa kubwa nchini kutokana na uwezo mkubwa wa kuwatoka mabeki na kufunga mabao alitarajia kuzikwa jana Wilaya ya Kisarawe, Mkoa wa Pwani.

Kwa mujibu wa mdogo huyo wa marehemu, Dilunga amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 62, ameacha mke na watoto sita.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Vodacom Premier League season to start August 23

Selikali yaidai posho TFF