in

Matembezi ya kumchangia Mtagwa leo

Nyota wa zamani wa soka nchini leo wanatarajia kufanya matembezi ya hisani kwa ajili ya kukusanya fedha za kumsaidia nyota wenzao, Jella Matagwa anayesumbuliwa na maradhi ya kupooza.

Matembezi hayo ya kumchangia Mtagwa aliyewahi kuwika na timu za Yanga, Pan Afrika na Taifa Stars, yamepangwa kuanzia Magomeni na kumalizika kwenye Hoteli ya Friend’s Corner, Manzese ambapo ndipo watakapoukabidhi msaada huo.

Akizungumza jana jijini Dar, Mratibu wa Matembezi hayo, Paul Lusozi ‘Father’, alisema zaidi ya nyota 40 wa zamani na wa sasa watashiriki katika matembezi hayo.

“Tunashukuru wengi wamethibitisha kushiriki matembezi haya, kwa kweli ndugu yetu (Mtagwa) anahitaji msaada kutokana na hali yake ya kupooza mwili, tumepanga kukutana kwenye hoteli hiyo na kukabidhi msaada wetu kwa kuwa nyumba yake ipo karibu na eneo hilo,” alisema Lusozi.

Kwa mujibu wa Lusozi, msaada watakaoukabidhi kwa Mtagwa ni pamoja na fedha taslimu kwa ajili ya kumsaidia kwenye matibabu yake na familia yake kwa ujumla.

Aidha, alisema kuna haja kwa serikali kuwatafuta na kuwasaidia wachezaji wenye matatizo kama akina Mtwaga ambao walijitolea kulisaidia taifa enzi zao.

Alisema, wachezaji wa zamani waliweka mbele uzalendo na maslahi ya taifa mbele tofauti na ilivyo sasa ambapo soka limekuwa biashara, hivyo kuwafanya waishi maisha duni.

Alisema mpango wa kuwakumbuka wachezaji wa zamani wenye matatizo mbalimbali unatarajiwa kuendelea kufanywa jijini Arusha kumchangia fedha Alain Shomari anayesumbuliwa na tatizo la macho na Badi Saleh aliyekatwa mguu kutokana na tatizo la maradhi ya kisukari anayeishi Sinza, Dar.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

January transfer window shopping list…..

Yanga yatakiwa kuacha nyodo Zanzibar