in , , , ,

Manchester United wamnasa Shaw

Manchester United wamemsajili beki wa kushoto wa Southampton na Timu ya Taifa ya England, Luke Shaw
United wanaelezwa kwamba wamemsajili mlinzi huyo kwa kitita cha pauni milioni 27, ikiwa ni baada ya Mwingereza huyo kuwaambia Saints juu ya tamaa yake ya kuchezea Man U.
Shaw (19) ni mchezaji mzuri na malipo ya dili lake yanasemwa yanaweza kuongezeka hadi pauni milioni 31 kutegemeana na ufaisi wake dimbani. Mei mwaka huu Saints walikataa dau la awali la pauni milioni 27 wakisema kwamba beki huyo alikuwa hauzwi.
Shaw amesainiwa kwa mkataba wa miaka minne ambapo kuna kipengele cha kuweza kuuongeza kwa mwaka mmoja zaidi.
Mwenyewe Shaw amesema kwamba anataka kujiendeleza kisoka akiwa na Man United kwa sababu anaamini ndiyo sehemu mwafaka kwake kuwa na kutekeleza ndoto hiyo.
Kocha Msaidizi wa Man U, Ryan Giggs amesema kwamba Shaw ni mchezaji mwenye kipaji cha hali ya juu na anatarajiwa kufanya makubwa katika siku zijazo kwenye ulimwengu wa soka.
Huyu ni mchezaji wa pili kusajiliwa na Man U baada ya Ander Herrera (24), Mhispania aliyechukuliwa kutoka Athletic Bilbao kwa ada inayokadiriwa kuwa pauni milioni 29.
Wayne Rooney alikuwa mchezaji mdogo zaidi kusajiliwa Old Trafford 2004 kwa pauni milioni 20, kwa hiyo usajili wa Shaw unampiga kumbo na unaendana na ule wa Marquihos aliyesajiliwa Paris St-Germain kutoka Roma Julai.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

‘Suarez anahitaji tiba’

Nigeria wagomea mazoezi