Fahamu Hadithi za Kuvutia Nyuma ya Kila Jina!
Utamu wa soka ni zaidi ya dakika tisini tu. Utani wa kawaida, wa jadi, na hata wa majina ya wachezaji au ya timu unachangia ladha ya mchezo huu. Katika Ligi Kuu ya England, majina ya utani ya vilabu vya soka yana historia ndefu na ya kipekee, yakiwa sehemu ya utambulisho wa kila klabu. Wakati mengine yanatokana na asili za miji, mengine yalitokea kwa bahati, lakini yote yanabeba hadithi za kipekee zinazostahili kusimuliwa.
Majina ya Utani ya Vilabu Vya Juu Vya Ligi Kuu
Tukianza na Arsenal, jina lao la utani ni βThe Gunnersβ au βWashika Bundukiβ, likihusishwa na wafanyakazi 15 kutoka kiwanda cha silaha cha Royal Arsenal huko Woolwich waliofanikisha kuanzishwa kwa klabu hiyo. Mashabiki wa Arsenal hujiita βGoonersβ, jina ambalo lina asili inayokinzana. Wengi wanaamini kuwa jina hili lilitokana na jina la βGunnersβ, likifupishwa ili kurahisisha matamshi.
Newcastle United wanajulikana kwa majina mawili maarufu: βToon Armyβ (kwa lafudhi ya Kaskazini-mashariki) na βMagpiesβ, jina linalohusishwa na rangi ya jezi yao nyeusi na nyeupe. Magpies ni aina ya ndege wenye rangi hizo, na nembo ya klabu hiyo iliwahi kuwa na picha ya ndege huyo kuanzia miaka ya 1970 na 1980.
Wanyama na Majina ya Utani
Vilabu vingine vimepata majina ya utani kutokana na wanyama na ndege. Kwa mfano, Leicester City wanaitwa βThe Foxesβ kutokana na nembo ya mbweha kwenye jezi yao, iliyoanza kutumika mwaka 1948. Hii ilitokana na uwindaji wa mbweha, tukio maarufu katika eneo la Leicestershire.
Ipswich Town wanaitwa βThe Tractor Boysβ, jina la hivi karibuni lililoanza mwishoni mwa miaka ya 1990. Eneo la Suffolk lina urithi wa kilimo, na jina hili lilitolewa kama dhihaka na majirani zao kwa kuwaona kama klabu ya “watu wa mashambani.” Mashabiki wa Ipswich walilikubali jina hilo na kuanza kuimba kwa utani, “1-0 to the Tractor Boys.”
Chelsea walijulikana kama βThe Pensionersβ hadi miaka ya 1950, jina lililotokana na uhusiano wao na Hospitali ya Chelsea, ambayo ilihifadhi maveterani wa vita. Hata hivyo, meneja Ted Drake aliamua kubadilisha taswira ya klabu hiyo, akaondoa jina hilo na kutambulisha nembo mpya ya simba. Ingawa jina la utani la βThe Lionsβ lilionekana kufaa, tayari lilikuwa linatumika na wapinzani wao wa London, Millwall.
Liverpool wamekuwa wakijulikana kama βThe Redsβ tangu mwaka 1896 kutokana na rangi nyekundu ya jezi zao. Umaarufu wa jina hili uliimarika zaidi katikati ya miaka ya 1960 wakati kocha maarufu Bill Shankly alipobadilisha sare ya timu kuwa nyekundu kabisa.
Manchester United walianza kutumia jina la utani βRed Devilsβ kutokana na msukumo wa kocha Sir Matt Busby. Alihamasishwa na timu ya rugby ya Salford, ambayo ilitembelea Ufaransa wakiwa wamevaa mashati mekundu, na vyombo vya habari vya huko waliwapa jina la βLes Diables Rougesβ (Mashetani Wekundu).
Simulizi Zaidi za Majina ya Utani
Crystal Palace awali walijulikana kama βThe Glaziersβ kutokana na historia ya eneo lao la zamani la viwanda vya kioo. Hata hivyo, meneja Malcolm Allison katika miaka ya 1970 alibadilisha jina hilo na kutambulisha βThe Eaglesβ ili klabu hiyo iwe na jina lenye nguvu zaidi.
Hii ilisababisha wapinzani wao wakubwa, Brighton & Hove Albion, kubadilisha jina lao la utani. Awali walijulikana kama βThe Dolphinsβ, kutokana na mazingira ya bahari na kivutio cha ndege aina ya dolphin katika eneo hilo, lakini mashabiki walichagua jina la βThe Seagullsβ (Mabwawa), ambalo lilibaki hadi leo.
Nottingham Forest jina lao la utani limebaki βForestβ tangu walipocheza kwenye uwanja wa Forest Recreation Ground mwaka 1865. Klabu hiyo ilianzishwa katika pub moja iitwayo Playwright katika Mtaa wa Shakespeare, na walitumia jina la Giuseppe Garibaldi, mpiganiaji wa uhuru wa Italia.
Majina ya Utani yasiyo Maarufu Sana
Si kila jina la utani linafahamika sana kama βThe Gunnersβ au βThe Redsβ au βRed Devilsβ. Kwa mfano, Tottenham Hotspur wanaitwa βThe Lilywhitesβ kutokana na jezi yao nyeupe, jina lililoanza kutumika tangu mwaka 1898. Hata hivyo, jina la βSpursβ ndilo maarufu zaidi, likiwa ni kifupi cha jina la klabu.
Manchester City wanaitwa βThe Citizensβ au βThe Sky Bluesβ, kutokana na rangi ya jezi zao, huku Fulham wakijulikana kama βThe Cottagersβ, wakirejea makazi yao mapya ya Craven Cottage tangu mwaka 1896.
Southampton wanajulikana kama βThe Saintsβ, jina lililotokana na kuanzishwa kwa klabu hiyo katika kanisa la Southampton St Maryβs, huku Aston Villa wakiwa na majina matatu maarufu: βVillaβ, βThe Lionsβ, na βThe Villansβ, lililotokana na jina la klabu.
Vilabu Vya Ligi za Chini nazo Hazijapitwa na Majina ya Utani
Katika ligi za chini, majina ya utani mara nyingi yana asili ya viwanda vya miji. Kwa mfano, Stoke City wanajulikana kama βThe Pottersβ kutokana na historia ya ufinyanzi ya mji huo. Sheffield United wanaitwa βThe Bladesβ kutokana na tasnia ya chuma ya Sheffield, huku Northampton Town wakiitwa βThe Cobblersβ kutokana na utengenezaji wa viatu.
Sheffield Wednesday wanajulikana kama βThe Owlsβ, jina lililotokana na eneo la Owlerton. West Bromwich Albion wana majina mawili: βThe Throstlesβ, jina la ndege aina ya thrush, na βThe Baggiesβ, ambalo lina asili inayobishaniwa.
Kwa kuhitimisha majina ya utani ya vilabu vya soka vya England hayana tu maana ya kawaida, bali yanabeba historia na utambulisho wa miji, viwanda, na hata simulizi za watu mashuhuri. Kuanzia Gunners wa Arsenal hadi The Bees wa Brentford, kila jina lina simulizi yake ya kipekee, ambayo siyo tu inaongeza ladha kwa mashabiki, bali pia inaakisi utambulisho wa vilabu hivi kwa vizazi vyote.
Comments
Loading…