in , , ,

Majina ya Utani ya Vilabu Vya Soka vya England


Fahamu Hadithi za Kuvutia Nyuma ya Kila Jina!

Utamu wa soka ni zaidi ya dakika tisini tu. Utani wa kawaida, wa jadi, na hata wa majina ya wachezaji au ya timu unachangia ladha ya mchezo huu. Katika Ligi Kuu ya England, majina ya utani ya vilabu vya soka yana historia ndefu na ya kipekee, yakiwa sehemu ya utambulisho wa kila klabu. Wakati mengine yanatokana na asili za miji, mengine yalitokea kwa bahati, lakini yote yanabeba hadithi za kipekee zinazostahili kusimuliwa.

Majina ya Utani ya Vilabu Vya Juu Vya Ligi Kuu

Tukianza na Arsenal, jina lao la utani ni ‘The Gunners’ au ‘Washika Bunduki’, likihusishwa na wafanyakazi 15 kutoka kiwanda cha silaha cha Royal Arsenal huko Woolwich waliofanikisha kuanzishwa kwa klabu hiyo. Mashabiki wa Arsenal hujiita ‘Gooners’, jina ambalo lina asili inayokinzana. Wengi wanaamini kuwa jina hili lilitokana na jina la ‘Gunners’, likifupishwa ili kurahisisha matamshi.

Newcastle United wanajulikana kwa majina mawili maarufu: ‘Toon Army’ (kwa lafudhi ya Kaskazini-mashariki) na ‘Magpies’, jina linalohusishwa na rangi ya jezi yao nyeusi na nyeupe. Magpies ni aina ya ndege wenye rangi hizo, na nembo ya klabu hiyo iliwahi kuwa na picha ya ndege huyo kuanzia miaka ya 1970 na 1980.

Wanyama na Majina ya Utani

Vilabu vingine vimepata majina ya utani kutokana na wanyama na ndege. Kwa mfano, Leicester City wanaitwa ‘The Foxes’ kutokana na nembo ya mbweha kwenye jezi yao, iliyoanza kutumika mwaka 1948. Hii ilitokana na uwindaji wa mbweha, tukio maarufu katika eneo la Leicestershire.

Ipswich Town wanaitwa ‘The Tractor Boys’, jina la hivi karibuni lililoanza mwishoni mwa miaka ya 1990. Eneo la Suffolk lina urithi wa kilimo, na jina hili lilitolewa kama dhihaka na majirani zao kwa kuwaona kama klabu ya “watu wa mashambani.” Mashabiki wa Ipswich walilikubali jina hilo na kuanza kuimba kwa utani, “1-0 to the Tractor Boys.”

Chelsea walijulikana kama ‘The Pensioners’ hadi miaka ya 1950, jina lililotokana na uhusiano wao na Hospitali ya Chelsea, ambayo ilihifadhi maveterani wa vita. Hata hivyo, meneja Ted Drake aliamua kubadilisha taswira ya klabu hiyo, akaondoa jina hilo na kutambulisha nembo mpya ya simba. Ingawa jina la utani la ‘The Lions’ lilionekana kufaa, tayari lilikuwa linatumika na wapinzani wao wa London, Millwall.

Liverpool wamekuwa wakijulikana kama ‘The Reds’ tangu mwaka 1896 kutokana na rangi nyekundu ya jezi zao. Umaarufu wa jina hili uliimarika zaidi katikati ya miaka ya 1960 wakati kocha maarufu Bill Shankly alipobadilisha sare ya timu kuwa nyekundu kabisa.

Manchester United walianza kutumia jina la utani ‘Red Devils’ kutokana na msukumo wa kocha Sir Matt Busby. Alihamasishwa na timu ya rugby ya Salford, ambayo ilitembelea Ufaransa wakiwa wamevaa mashati mekundu, na vyombo vya habari vya huko waliwapa jina la ‘Les Diables Rouges’ (Mashetani Wekundu).

Simulizi Zaidi za Majina ya Utani

Crystal Palace awali walijulikana kama ‘The Glaziers’ kutokana na historia ya eneo lao la zamani la viwanda vya kioo. Hata hivyo, meneja Malcolm Allison katika miaka ya 1970 alibadilisha jina hilo na kutambulisha ‘The Eagles’ ili klabu hiyo iwe na jina lenye nguvu zaidi.

Hii ilisababisha wapinzani wao wakubwa, Brighton & Hove Albion, kubadilisha jina lao la utani. Awali walijulikana kama ‘The Dolphins’, kutokana na mazingira ya bahari na kivutio cha ndege aina ya dolphin katika eneo hilo, lakini mashabiki walichagua jina la ‘The Seagulls’ (Mabwawa), ambalo lilibaki hadi leo.

Nottingham Forest jina lao la utani limebaki ‘Forest’ tangu walipocheza kwenye uwanja wa Forest Recreation Ground mwaka 1865. Klabu hiyo ilianzishwa katika pub moja iitwayo Playwright katika Mtaa wa Shakespeare, na walitumia jina la Giuseppe Garibaldi, mpiganiaji wa uhuru wa Italia.

Majina ya Utani yasiyo Maarufu Sana

Si kila jina la utani linafahamika sana kama ‘The Gunners’ au ‘The Reds’ au ‘Red Devils’. Kwa mfano, Tottenham Hotspur wanaitwa ‘The Lilywhites’ kutokana na jezi yao nyeupe, jina lililoanza kutumika tangu mwaka 1898. Hata hivyo, jina la ‘Spurs’ ndilo maarufu zaidi, likiwa ni kifupi cha jina la klabu.

Manchester City wanaitwa The Citizens’ au The Sky Blues, kutokana na rangi ya jezi zao, huku Fulham wakijulikana kama ‘The Cottagers’, wakirejea makazi yao mapya ya Craven Cottage tangu mwaka 1896.

Southampton wanajulikana kama ‘The Saints’, jina lililotokana na kuanzishwa kwa klabu hiyo katika kanisa la Southampton St Mary’s, huku Aston Villa wakiwa na majina matatu maarufu: ‘Villa’, ‘The Lions’, na ‘The Villans’, lililotokana na jina la klabu.

Vilabu Vya Ligi za Chini nazo Hazijapitwa na Majina ya Utani

Katika ligi za chini, majina ya utani mara nyingi yana asili ya viwanda vya miji. Kwa mfano, Stoke City wanajulikana kama ‘The Potters’ kutokana na historia ya ufinyanzi ya mji huo. Sheffield United wanaitwa The Blades kutokana na tasnia ya chuma ya Sheffield, huku Northampton Town wakiitwa ‘The Cobblers’ kutokana na utengenezaji wa viatu.

Sheffield Wednesday wanajulikana kama The Owls’, jina lililotokana na eneo la Owlerton. West Bromwich Albion wana majina mawili: ‘The Throstles’, jina la ndege aina ya thrush, na The Baggies’, ambalo lina asili inayobishaniwa.

Kwa kuhitimisha majina ya utani ya vilabu vya soka vya England hayana tu maana ya kawaida, bali yanabeba historia na utambulisho wa miji, viwanda, na hata simulizi za watu mashuhuri. Kuanzia Gunners wa Arsenal hadi The Bees wa Brentford, kila jina lina simulizi yake ya kipekee, ambayo siyo tu inaongeza ladha kwa mashabiki, bali pia inaakisi utambulisho wa vilabu hivi kwa vizazi vyote.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

17 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0
Tanzania Sports

Tunatamani Yanga iwe “Man City”

Tanzania Sports

“Simba lazima ishinde”-Ahmed Ally