in

Kikapu nao wataka kocha `mzungu`

Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania, TBF, limemuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete nao kuwaletea kocha wa kigeni kwa ajili ya kuinoa timu ya taifa ya mchezo huo.

Kauli ya TBF imekuja baada ya Kikwete katika hotuba yake kwa Wabunge wiki iliyopita kuwaahidi wadau wa riadha kuletewa kocha wakigeni kama alivyofanya kwa timu ya taifa ya soka.

Rais wa TBF Richard Kasesera alisema katika suala hilo nao wanaomuomba rais awaletee makocha hata wa kujitolea ili waweze kuwasaidia kutengeneza timu itakayokuwa ikishiriki michuano mbalimbali ya kimataifa.

“Tunamuomba rais atusaidie na TBF, sababu suala la kocha ni tatizo sugu katika chama hicho,“ alisema Kasesera.

Aliongeza kusema kwa upande wa mchezo wa kikapu, wanashindwa hata kushiriki katika michuano ya Olimpiki, kutokana na kukosa kocha ambaye atainoa timu ya taifa, itakayoshiriki michuano ya kikapu.

Wakati huo huo, Kasesera aliupongeza mkoa wa Dar es Salaam kuandaa mashindano ya kikapu ya shule za Sekondari yanaoendelea katika uwanja wa ndani wa taifa.
Akizungumza jana, alisema michuano hiyo inasaidia kupata wachezaji chipukizi watakaojiunga katika timu ya taifa ya baadae.

  • SOURCE: Nipashe

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Tunasibiri majaliwa ya Kikwete katika riadha Tanzania

Bayi, Nyambui ni Alfa na Omega Olimpiki?