in

Kiingilio cha kuwaona stars Mwanza ni mzigo kwa wananchi!

KIINGILIO cha mechi ya timu ya Tanzania,Taifa Stars na Uganda, The Cranes, itakayochezwa leo kwenye Uwanja wa CCM Kirumba kimelalamikiwa na mashabiki wa soka hapa kuwa ni kikubwa.

Shirikisho la soka Tanzania, TFF limetangaza kuwa watakaotaka kuuona mchezo huo watalazimika kulipa sh,5,000 kwa mzunguko na sh,20,000 kwa jukwaa kuu.

Nizar Khalfan

Baadhi ya mashabiki wameanza kugwaya na kupanga kuusikiliza mchezo huo kupitia redio na kwa kile walichodai kuwa kiingilio ni kikubwa.

Taarifa mbalimbali zilizokuwa zikipatikana jijini humo kutoka kwa mashabiki na wapenzi wa soka tangu kutangazwa kwa kiingilio hicho zilikuwa zinasema kwamba kiingilio hicho ni kikubwa mno kiasi kwamba mashabiki wengi hawataweza kumudu hali ambayo inaweza kupunguza mapato kwa timu hizo.

Msemaji wa TFF nchini Florian Kaijage aliviomba vyombo vya habari jana jijini hapa kuwaelimisha wapenzi wa soka kuwa hicho ni kiingilio cha kawaida kutokana na gharamaza uendeshaji wa mechi hiyo.

Kaijage alisema kuwa kiingilio hicho sio mara ya kwanza kutumika kwa mechi kubwa katika jiji la Mwanza ispokuwa vyombo vya habari vinatakiwa kusidia TFF kuwaelimisha wapenzi ili wajitokeze kwa wingi.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Superb O’Sullivan completes Hendry job

Premier League – Ten-man United romp past Hammers