Katika hali ya kushangaza, Guinea ya Ikweta iliyokuwa imefutwa kwenye michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2015, imeteuliwa kuwa nchi mwenyeji na timu yake itashiriki.

Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) limefikia uamuzi huo baada ya waliokuwa wawe wenyeji, Morocco kukataliwa ombi la kuahirishwa michuano hiyo kutoka Januari 17 hadi Februari 8 mwakani kwa hofu ya kusambaa kwa maradhi hatari ya Ebola yaliyoua zaidi ya watu 5,000 Afrika Magharibi.

Rais wa CAF, Issa Hayatou ametangaza uamuzi huo baada ya kukutana na Rais Teodoro Obiang jijini Malabo, Guinea Ijumaa hii na rais kukubali serikali ya taifa lake kubeba msalaba huo.

Guinea walioandaa michuano hiyo pamoja na Gabon 2012 sasa watakuwa wenyeji pekee, na walikuwa wametolewa katika hatua za awali kwa madai ya kuchezesha mchezaji asiyekuwa na sifa walipocheza na Mauritania Mei 17 mwaka huu.

Morocco wametupwa nje ya mashindano hayo moja kwa moja, itabidi wajipange upya kwa ajili ya kufuzu kwenye inayokuja. Mashindano ya mwakani yanashirikisha timu 16.

“Mkuu wa Taifa la Guinea ya Ikweta amekubali kuwa mwenyeji wa michuano hiyo, kwa hiyo Kamati ya Utendaji ya CAF inatangaza kwamba mashindano yataendelea kama yalivyopanga na Guine ya Ikweta itashiriki kama nchi mwenyeji.

“Caf inapenda kutoa shukurani zake za dhayi kwa watu wa Guinea ya Ikweta, serikali yao na kwa namna ya pekee Rais Obiang,” akasema Hayatou kwenye taarifa yake.

Mechi zitachezwa katika miji ya Bata, Ebebiyin, Mongomo na mji mkuu wal Malabo. Mwaka 2012 ni viwanja vya Malabo na Bata tu vilitumiwa. Droo kwa ajili ya fainali hizo zitapangwa Malabo Desemba 3.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Qatar wasafishwa na rushwa

Mancini bosi mpya Milan