Menu
in

Ghana yatolewa jasho na Guinea

Ghana walilazimika kusubiri hadi dakika za mwisho kabla ya kuilaza Guinea mabao 2 kwa 1 katika mechi ya ufunguzi wa mashindano ya kombe la mataifa ya Afrika, mjini Accra.

Nchi kumi na sita zinashiriki katika mashindano hayo.

Mchezaji wa Black Stars, Sulley Muntari alitimua kombora kutoka futi 25 hadi wavuni ikiwa zimesalia dakika mbili peke yake mechi kumalizika.

Hivyo basi mshambulizi huyo ambaye pia huchezea kilabu ya Ligi Kuu ya Uingereza ya Portsmouth akaiondolea aibu nchi yake ambayo hapo awali iliichukulia Guinea kuwa mteremko.

Black Stars walikuwa wa kwanza kupata bao wakati Asamoah Gyan alivuna penalti mnamo dakika ya 54.

Lakini Guinea walionyesha machachari na usumbufu kiasi cha kusawazisha kupitia Oumar Kallabane.

Habari hii kwa hisani ya Bbc London.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version