in , , ,

Barcelona wawachapa Bayern 3-0

 

Barcelona wameonesha umwanba wao kwa kuwanyuka Bayern Munich 3-0 katika mechi ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL).

 

Kocha wa zamani wa Barca, Pep Guardiola alikuwa akirudi nyumbani katika timu aliyochezea, kufundisha na kupata nayo mataji, lakini ameduwazwa.

 

Hali ilikuwa shwari mwanzoni, ikitarajiwa kwamba walau wangekwenda suluhu, lakini balaa kwa wageni ilianza kipindi cha pili, kwani kunako dakika za 77 na 80 Messi alionesha ufalme wake, kisha Neymar akamalizia dakika ya mwisho ya mchezo.

 

Hata hivyo ilikuwa mechi ngumu, kwani hadi dakika 13 za mwisho mambo yalikuwa suluhu. Ilikuwa ni mechi muhimu na kali iliyeompeleka Guardiola kwenye klabu aliyochezea na kufundisha na kuwapa mataji mengi, yakiwamo ya Ulaya.

 

Katika nusu fainali nyingine Jumanne wiki hii, Juventus wamewaduwaza mabingwa wa Ulaya – Real Madrid kwa kuwafunga 2-1.

 

Barca wanaoufindishwa na mchezaji wao wa zamani, Luis Enrique aliyecheza na Guardiola hapo walijihisi katika hali nzuri, ambapo pia wanaongoza katika Ligi Kuu ya Hispania, maarufu kama La Liga.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Mourinho ataka sura mpya Chelsea

Mzozo Hispania: Soka yaahirishwa