in , , , ,

Amorim aisifu ‘mashine ya kazi’ Mbeumo


afunga mara mbili katika ushindi wa 4-2 dhidi ya Brighton
‘Anazidi kuboresha eneo la mwisho tunapopanga mashambulizi’

Ruben Amorim alimsifia Bryan Mbeumo, “mashine ya kazi,” aliyefunga mabao mawili, na akasisitiza umuhimu wa ushindi wa tatu mfululizo wa ligi baada ya Manchester United kushinda 4-2 dhidi ya Brighton katika uwanja wa Old Trafford, Jumamosi.

Mabao ya kipindi cha kwanza kutoka kwa Matheus Cunha na Casemiro yalifuatiwa na Mbeumo kuongeza la tatu baada ya mapumziko. Lakini United waliingia hofu baada ya Danny Welbeck na Charalampos Kostoulas kupunguza tofauti — huyu wa pili akifunga katika muda wa nyongeza kabla ya Mbeumo kukamilisha ushindi wake binafsi karibu na mwisho wa mchezo.

Tanzania Sports

Amorim aliulizwa kuhusu umuhimu wa Mbeumo na nafasi yake katika kumsajili kipindi cha kiangazi. “Yeye ni mashine ya kazi. Ni mzuri sana katika mashambulizi ya kushtukiza. Anazidi kuboresha tunapopanga mashambulizi katika eneo la mwisho,” alisema kocha huyo, kabla ya kumsifia kwa ushirikiano wake na Amad Diallo kwenye winga ya kulia. “Ni vigumu sana kuwapita hawa wawili kwa sababu hubadilishana nafasi, wana kasi sana, na ni wazuri sana katika mapambano ya mtu kwa mtu.”

“Kazi yangu ilikuwa ni kumuelekeza kile ninachotaka kutoka kwake kama meneja, lakini ilikuwa zaidi kazi ya klabu na ninyi [wanahabari]. Tunaweza kupitia kipindi kigumu, lakini hii ni Manchester United. Wakati United ipo na tunapohisi kwamba mchezaji anataka kuja hapa — haijalishi nafasi, haijalishi kama tuna Champions League au la — tunafanya kila kitu kumpata aina ya wachezaji kama hawa, na hivyo ndivyo ilivyokuwa.”

United walipanda hadi nafasi ya nne kutokana na Liverpool kupoteza dhidi ya Brentford. Amorim aliulizwa kuhusu klabu kushinda mechi tatu mfululizo za Premier League kwa mara ya kwanza tangu Februari 2024. “Ilikuwa muhimu sana — pia kwa sababu ya kiwango,” alisema. “Tuliteseka kidogo mwishoni, lakini isingekuwa Manchester United bila mateso kidogo. Lakini naamini tulistahili ushindi dhidi ya timu nzuri sana. Nafikiri wachezaji wangu wanajiamini zaidi sasa.”

Kuhusu bao la kwanza la Cunha akiwa na United, Amorim alisema: “Unaweza kuhisi kwamba alilitaka sana. Ninapenda sana jinsi alivyopambana leo. Alicheza vizuri sana, na anapokuwa na mpira si jambo linalonipa faraja sana.

Kwa upande mwingine, Fabian Hürzeler aliulizwa kuhusu tukio la Luke Shaw kumchezea rafu mbaya Georginio Rutter katika maandalizi ya bao la tatu la United. “Sitawahi kumlaumu mwamuzi kwa ajili ya kushindwa kwetu,” alisema meneja wa Brighton. “Tunahitaji kuboresha kiwango chetu wenyewe.

“Ni rahisi kuielezea mechi hii — tulifanya makosa mengi sana. Tulitoa mipira kirahisi, tulikuwa na udhibiti wa mchezo, tulifanya mashambulizi mazuri na tulikuwa hatari kila mara kwenye eneo lao, lakini ukifanya makosa ya kitoto na kutoa zawadi nne [kwa mabao], huwezi kushinda mechi.”

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0
Tanzania Sports

Brentford waidhalilisha Liverpool vibonde..

Tanzania Sports

Arsenal waongoza EPL kwa alama nne..