*Sare zaendelea, Gabon wachapwa

WAKATI sare zikitawala mechi tatu za katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), washabiki wamekabiliana na polisi kabla ya mechi baina ya wenyeji Guinea ya Ikweta na Burkina Faso.
Wakitaka kushabikia timu yao ya nyumbani, mamia ya washabiki walitaka kulazimisha kuingia uwanjani, huku wengine wakiwa hawana tiketi, baada ya kuzuiwa baadhi wakaanza kurusha mawe na polisi wakajibu kwa kufyatua mabomu ya kutoza machozi kwenye Uwanja wa Bata.

Polisi wamekuwa wakimiminika kwenye viwanja kwa ajili ya kuhakikisha usalama kwenye michuano hii, ambapo washabiki wamekuwa wakicheleweshwa kuingia uwanjani, ambapo hutokea kiwanja kimoja kikawa na mechi mbili zinazofuatana.
congogabon

Polisi wa kutuliza ghasia pia walilazimika kutumia ngumu kudhibiti wafuasi kwenye jiji la Ebebiyin katika mechi za kwanza. Guinea wanaandaa michuano hii kwa notisi ya dharura baada ya Morocco kuchelea kuandaa kwa hofu ya maradhi ya Ebola yaliyozikumba nchi za Liberia na Sierra Leone na kuua maelfu ya watu.

Katika mechi za Jumatano hii, Guinea ya Ikweta walikwenda suluhu na Burkina Faso, ikiwa ni sare ya pili kwa wenyeji huku Wabukinabe wakiwa wameambulia pointi moja katika mechi mbili.
Kwenye mechi nyingine Kongo Brazzaville waliwafunga Gabon bao 1-0, Ivory Coast wakatoshana nguvu 1-1 na Guinea Bissau huku Mali nao wakitoka nguvu sawa na Cameroon kwenye mechi za Jumanne.
Alhamisi hii Zambia wanacheza na Tunisia huku Visiwa vya Cape Verde wakicheza na Kongo Kinshasa.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

TETESI ZA USAJILI LEO

JE SIKU HIZI NI TABIA AU FEDHA NDIYO MUHIMU KATIKA MICHEZO?