in

ZFA yadaiwa kuibeba Miembeni

Chama cha soka cha Zanzibar, ZFA, kimeshutumiwa kuwa kimekuwa kikipangua mara kwa mara ratiba ya ligi kuu ya Zanzibar ili kuiweka timu ya Miembeni katika mazingira mazuri ya kutetea ubingwa wake.

Aidha, ZFA imelaumiwa pia kuwa na njama za kuipendelea Malindi kwa kumpanga mwamuzi mmoja aliyetajwa kwa jina la Kisaka kuchezesha mechi zote za timu hiyo.

Kocha mkuu wa timu ya Mundu na mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Zanzibar Hemed Morocco aliliambia Lete RAHA kwa njia ya simu katikati ya wiki kuwa kwa sasa hakuna haki katika soka visiwani kutokana na ZFA kuzikumbatia baadhi ya timu ili zitwae ubingwa, na nyingine zibaki katika ligi hiyo.

“Tunaomba mtusaidie hawa wenzetu hakuna wanachofanya zaidi ya malumbano yasiyokuwa na msingi, sasa hakuna soka kabisa Zanzibar, yaani ungeona mechi yetu na Malindi kama kweli ni mpenzi wa soka hutapenda kabisa kuja tena uwanjani kutazama, waamuzi wanafanya madudu ya wazi wakipendelea timu hizo,“ alisema Morocco.

Mundu imeongoza ligi kuu kwa muda mrefu na pamoja na Miembeni ndiyo zenye uwezekano mkubwa wa kutwaa ubingwa.

Alisema Malindi imecheza mechi moja pungufu baada ya mchezo dhidi ya KMKM kuahirishwa na haijulikani utachezwa lini.

Hatahivyo, alisema pamoja na hujuma zote wanazofanyiwa bado wana uhakika wa kuwavua ubingwa Miembeni kutokana na ubora wa timu yake ambao hautegemei kubebwa na mwamuzi.

Malindi iliyokuwa kwenye janga la kushuka daraja imechupa kutoka nafasi ya 10 hadi ya saba baada ya kushinda mechi sita na kutoka sare mara tano katika michezo 17. Timu nne, kati ya 12, zitashuka daraja kwa mujibu wa kanuni.

  • SOURCE: Lete Raha

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Euro 2008 – Spot on Spain knock out Italy

Premier League – Arsenal complete Nasri signing