in

Wageni wafurika Azam Fc

BENCHI la ufundi la Azam Fc limesema hakutakuwa na mapumzika kwa wachezaji wakati wa mapumziko ya Ligi Kuu na tayari wachezaji saba wa kigeni toka Uganda, Kenya na Msumbiji wameshawasili kufanya majaribio na kikosini hicho.

Azam ambayo ni msimu wake wa kwanza kushiriki Ligi Kuu ya Bara, haikufanya vizuri kwenye mzunguko wa kwanza uliomalizika hivi karibuni kwa madai kuwa hawakuwana muda wa maandalizi kabla ya ligi kuanza.

Kocha msaidizi wa timu hiyo, Sylvester Marsh aliiambia Mwananchi jana kuwa wachezaji saba wa kigeni tayari wameshatua kwenye timu hiyo na kuanza mazoezi lakini wiki ijayo watawatolea tamko.

“Sisi ni kama hatuna timu, hatukufanya vizuri sana kwenye mzunguko wa kwanza kwa vile muda wa maandalizi ulikuwa kidogo sana na ndio maana tumeamua kwamba hakuna likizo, tutawapa siku chache sana wiki zijazo,” alisema Marsh ambae aliwahi kuinoa Kagera Sugar kwa mafanikio.

“Tumeandaa programu nzito ambayo katika huu muda wote wa mapumziko timu itatengamaa vizuri, tayari Wakenya watatu, Msumbiji wawili na Waganda wawili wameshatua kwenye timu yetu.

“Rekodi zao zinaonyesha ni wachezaji wazuri, lakini tunawafanyia majaribio kwanza tuwaone mpaka wiki ijayo tutajua nini cha kufanya, hatujapata uhakika tuna nafasi ngapi za kujaza kwa vile kuna mambo yanaendelea kwenye uongozi,” alisema kocha huyo ambaye bosi wake ni Neider dos Santos wa Brazil.

“Kuna wachezaji tutawarudisha kwenye timu zao za daraja la kwanza, wengine tutawauza Ligi Kuu kuna makubaliano yanaendelea yakishamalizika ndio nafasi zao tutajaza muda si mrefu.”

Marsh ambae aliwahi kuinoa timu ya Taifa ya Vijana, Serengeti Boys alisema kiungo mshambuliaji wa APR ya Rwanda, Haruna Nyiyonzima anatazamiwa kutua nchini siku yoyote kuanzia leo huku Mganda, Danny Wagaluka wa URA wameshamalizana naye na amerudi kwao.

“Wagaluka tumeshamalizana naye na atarudi nchini siku si nyingi, kuna wageni wengine wataongezeka kwa majaribio pia siku si nyingi,”alisema kocha huyo ambaye timu yake imemaliza mzunguko wa kwanza ikiwa nafasi ya nane na pointi 13.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Champions League – Arsenal held by Fenerbahce

Premier League – Team news: Arsenal crisis