Menu
in

Twiga Stars yatinga nusu fainali COSAFA

Timu ya taifa ya soka ya wanawake, Twiga Stars, imetinga katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara (COSAFA), baada ya kuifunga Zambia 2-0 katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Gwanzura hapa Zimbabwe.

 

Kwa ushindi huo, Twiga Stars imefikisha pointi sita baada ya juzi Jumamosi kuwafunga Botswana 3-1.

Twiga sasa itacheza mechi ya mwisho ya hatua ya makundi ya kukamilisha ratiba dhidi ya Afrika Kusini Jumatano.

Katika mechi ya jana, Twiga, ambayo imealikwa katika michuano hiyo baada ya kufanya vyema katika michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wanawake iliyofanyika nchini Afrika Kusini mwaka jana, magoli yote mawili yalifungwa na mshambuliaji Asha Rashid ‘Mwalala’ katika dakika za 21 na 33.

Mechi za hatua ya nusu fainali zitachezwa Alhamisi Julai 7

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version