Menu
in

Timu nane zawasili Dar kwa michuano ya netiboli

TIMU za mataifa nane zimewasili nchini tayari kwa mashindano ya kimataifa ya netiboli ya ‘Inter Nations Netball Tounament’, yatakayoanza kesho kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam.

Mashindano hayo ambayo yanashirikisha nchi 10 kutoka Afrika Tanzania imepangwa kuvaana na Lesotho katika mchezo wa Ufunguzi kesho.

Mwenyekiti wa Chaneta, Anna Bayi alisema timu hizo zitafikia katika Hotel ya Blue Pearl na Land Mark zilizopo Ubungo ambapo wachezaji na viongozi wao watakaa.

Alisema maandalizi kwa asilimia kubwa yamekamilika na timu ipo katika hali nzuri kimchezo na kiafya na kuahidi kufanya vizuri katika mashindano hayo.

Nchi zilizowasili ni pamoja na Afrika Kusini,Zimbabwe pamoja na Swazland. Tanzania imepangwa kundi A na nchi za Namibia,Zimbabwe na Afrika kusini.

Kundi B zipo nchi za Kenya, Uganda, Malawi, Zambia na Swaziland ambapo pazia litafunguliwa kati ya Malawi na Kenya.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version