in

TFF kujadili miaka minne ya utawala wao

SHIRIKISHO la Soka Tanzania, TFF, limeanza harakati za kujiandaa na mkutano mkuu mwezi Desemba na sasa limeandaa kongamano la siku tatu kwa wadau wa soka kuzungumzia mkutano huo..

Mkutano mkuu wa shirikisho hilo utafanyika mapema mwezi Desemba ukifuatiwa na uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo chini ya uongozi wa Leodegar Tenga na Makamu wake, Crescentius Magori unamaliza muda wake.

Uongozi huo wa Tenga uliingia madarakani Desemba 28, 2004 na tayari vuguvugu kwa ajili ya uchaguzi huo limeanza kufukuta huku aliyekuwa katibu mkuu wa shirikisho hilo ambaye aliangushwa na Tenga kwenye uchaguzi wa mwaka 2004 Michael Wambura kukiwa na tetesi kuwa atawania nafasi ya juu kwenye uchaguzi huo wa Desemba.

Likiwa linajipanga kwa ajili ya uchaguzi huo, shirikisho hilo limeandaa Kongamano kwa wadau wa soka ambalo litafayika Septemba 18 hadi 20 kwenye Ukumbi wa NSSF Water Front jijini Dar es Salaam.

Kongamano hilo ambalo limeandaliwa na TFF kwa kushirikiana na Chama cha Makocha Tanzania (TAFCA), lina lengo la kutathmini mwenendo mzima wa soka ya Tanzania tangu uongozi wa Tenga ulipoingia madarakani mpaka hivi sasa.

Katibu Mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela alisema kongamano hilo litakuwa la kitaifa na litakalotoa nafasi kwa wadau kutoa maoni yao ya nini kifanyike ili kukuza na kuendeleza soka ya Tanzania.

“Kongamano hili litaeleza nafasi ya makocha, waamuzi na madaktari wa michezo katika maendeleo ya soka,” alisema Mwakalebela.

Alisema: ”TFF pia tutaweka wazi matarajio yetu masuala mazima ya fedha, na vyanzo mbali mbali vinavyotuingizia pesa ikiwa ni pamoja na mikakati yetu katika kuhakikisha TFF inajiwezesha yenyewe katika masuala mazima ya fedha pamoja na miundo mbinu kwa maana ya viwanja.”

Kongamano hilo limepangwa kufunguliwa na Naibu Waziri wa Habari na Utamaduni Joel Bendera na litafungwa na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Idd Kipingu.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Walcott feat a ‘one-off’ – Wenger

Liverpool v Man Utd