in

Tanzania yaanza vibaya Olimpiki

Tanzania jana ilianza vibaya Michezo ya 29 ya Olimpiki inayofanyika Beijing, China baada ya waogeleaji wake kutupwa nje ya michezo hiyo.

Katika mchezo wa kuogelea Tanzania iliwakilishwa na wachezaji wawili ambao ni Khalida Rushaka kwa upande wa wanaume na Magdalena Alex Moshi kwa upande wa wanawake, ambao wote kwa pamoja walikuwa wakiogelea aina moja ya mitindo huru `Free Style` mita 100.

Waogeleaji hao wameshindwa kufurukuta baada ya kukutana na wataalamu wa kuogelea, ambapo Moshi alishindwa hata kuingia hatua ya pili huku Rushaka akitupwa nje ya mchezo huo kama ilivyokuwa kwa mwenzake.

Kwa upande wa wanawake Coughlin Natalia wa Marekani aliweza kushika nafasi ya kwanza na kujihakikishia kucheza fainali leo huku Trickett Lisbeth kutoka Australia akishika nafasi ya pili na nafasi ya tatu ilikwenda kwa Vingwen Zhu wa China.

Kwa upande wa waogeleaji wanaume mitindo huru Suillivan Eamon wa Australia aliweza kushika nafasi ya kwanza na kujihakishia hatua ya fainali huku Vanden Hoogen Band Pieter wa Netheland aliweza kuchukua nafasi ya pili na nafasi ya tatu ilikwenda kwa Targett Matt wa Australia.

Tanzania itajaribu tena bahati yake siku ya Jumapili kwa wanariadha wake wa mita 10,000, Samwe Kwang`w , Dickson Marwa na Fabian Joseph kuanza kuanza kufukuza upepo, ambapo matumaini makubwa ya watanzania yatakuwa hapo.

Katika michezo hiyo Tanzania imewakilishwa na timu mbili ambazo ni ya kuogelea na timu ya riadha, ambapo hadi sasa haijafanikiwa kupata medali hata moja huku Zimbabwe ikiongoza kwa upande wa timu za Afrika kwa kujinyakulia medali tatu za shaba kwa upande wa waogeleaji.

  • SOURCE: Nipashe

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Champions League – Lacklustre Arsenal beat Twente

Premier League set for kick-off