in

Taifa Queens warejea vichwa chini

Mchezaji wa Timu ya taifa ya netiboli, Taifa Queen akifunga.

Timu ya taifa ya netiboli, Taifa Queens, imerejea juzi ikitokea nchini Uingereza ambako ilienda kwa ajili ya kucheza mechi za kirafiki na nchi za huko.

Kikosi hicho ambacho kiliondoka na wachezaji tisa, kimeshindwa kufanya vizuri kutokana na kuwa na majeruhi wengi.

Akizungumza mara baada ya kikosi hicho kuwasili, mratibu wa safari hiyo, Joel Mwakitalu, alisema kuwa wamejitahidi lakini tatizo la majeruhi liliwaathiri sana.

“Tumeshindwa kufanya vizuri kutokana na kukabiliwa na majeruhi,” alisema Mwakitalu.

Aliongeza kuwa pamoja na kushindwa kurejea na kombe lakini wamejifunza mengi ikiwemo kupata uzoefu wa kucheza na timu ambazo zinashiriki michuano mikubwa ya netiboli duniani.

Alisema pia kuwa wachezaji wamefurahia ziara hiyo, ambayo imewajenga kisaikolojia.

Naye kocha wa timu hiyo, Mary Protasi, alisema kuwa somo walilopata wachezaji wake katika mechi hizo ni kubwa na litawasaidia sana watakapokutana na timu nyingine katika michezo ijayo. Timu iliondoka nchini wiki mbili zilizopita.

CHANZO: NIPASHE

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Fulham 2 – 1 Hamburg (agg 2 – 1)

Steve McClaren on verge of history with FC Twente