in , , ,

Sunderland wawachapa Man United

Manchester United wamepoteza mechi ya tatu mfululizo na kutia shinikizo kubwa kwa kocha David Moyes aliyemrithi Sir Alex Ferguson.

Safari hii Mashetani Wekundu wamefungwa na Sunderland wanaoburura mkia wa Ligi Kuu ya England (EPL), na ilikuwa kwenye mechi ya Kombe la Ligi (Capital One Cup).

Sunderland walifarijika kwa ushindi wa mabao 2-1 kutokana na mkongwe wa Man U Ryan Giggs kujifunga mwenyewe dakika ya 45, Nahodha Nemanja Vidic akasawazisha dakikaya 52 lakini Fabio Borini akapeleka simanzi United kwa bao la penati katika dakika ya 64.

Hii ni mara ya kwanza tangu 2001 kwa United kupoteza mechi tatu mfululizo na Moyes ameendeleza lawama zake kwa waamuzi, akisema penati waliyopewa Sunderland haikuwa halali.

Kadhalika ni mara ya kwanza kwa Sunderland kuwafunga United tangu mwaka 2000 katika mechi 21 baina yao. Borini anacheza Sunderland kwa mkopo kutoka Liverpool.

Timu mbili hizo zitarudiana Januari 22 baada ya United kuwa wameshatolewa kwenye Kombe la FA kwa kufungwa na Swansea na katika EPL wapo pointi 11 nyuma ya vinara Arsenal.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Kombe la FA: Arsenal na Coventry

Kombe la Dunia Qatar Novemba – Desemba