in

Serikali iangalie Chuo cha Michezo Malya- Kamati

KAMATI ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii imeitaka serikali iongeze bajeti kwa Chuo cha Maendeleo ya Michezo cha Malya mkoani humu ili kiweze kuboresha miundombinu yake na kutoa taaluma bora kwa walimu na makocha wa michezo nchini.

Kamati hiyo ilitoa ushauri huo mwisho wa wiki ilipofanya ziara ya siku moja katika chuo hicho kilichopo mkoani Mwanza.

Wajumbe wa kamati hiyo walikitembelea chuo hicho ili kujionea miundombinu yake na kutoa ushauri kwa serikali jinsi ya kukiboresha.

Katika majumuisho ya ziara yao, kamati hiyo chini ya kaimu mwenyekiti wake, Florence Kyendesya,

kamati hiyo ilimweleza Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Joel Bendera kuwa serikali inapaswa kukiangalia chuo hicho.

Wameshauri ijenge bwalo la chakula, ofisi ya

utawala, viwanja zaidi vya michezo vinavyoendana na hadhi ya chuo hicho.

Mjumbe wa kamati hiyo, Kapteni John Komba

alisema: “Serikali iangalie upya bajeti ya chuo hiki

kama kweli inataka kukiendeleza kwa kuimarisha bajeti yake kila mwaka ili kukikuza katika kiwango cha kimataifa.

Tukifanya hivyo, tutavutia watu wengi zaidi kuja

hapa na tutapata walimu wazuri watakaosaidia kuinua vipaji vya vijana wetu na wengine watakwenda nje na kuliletea taifa tija, alisema.

Aidha, wajumbe hao waliushauri uongozi wa chuo kuwa na mipango inayolenga katika kuinua vipaji vya vijana kwa kuwapatia mafunzo mazuri vijana wanaoletwa chuoni hapo.

Kwa mujibu wa wajumbe hao, chuo kinatakiwa kiandae mpango wa kuendeleza vijana kwa kuanzisha shule za msingi na sekondari zitakazochukua vijana wenye vipaji ili kuwawia rahisi kuibua vipaji kwa vya wanamichezo.

Kwa upande wake, Bendera aliwahakikishia wajumbe hao kuwa maoni yao serikali itayafanyia kazi na kuwa nia yake ni kukifanya Chuo cha Malya kuwa cha kisasa duniani katika siku zijazo.

Alisema: Nia ya serikali ni kuwa na chuo

cha kisasa hapa Malya kinachotoa mchango wa maendeleo ya michezo duniani.

Tumeanza na hivi sasa tunakamilisha ujenzi wa uwanja wa kisasa zaidi wa ndani katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati kwa gharama ya Shilingi 1,056,000,000 na kwamba tayari serikali imekamilisha ujenzi wa maktaba na kituo cha kompyuta.

Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya kilichoanzishwa na serikali mwishoni mwa miaka ya 1990, ndicho chuo pekee cha michezo kusini mwa Jangwa la Sahara kinachotoa stashahada ya

ufundishaji michezo. Tangu kuanzishwa kwake kimekwishatoa wahitimu 62 katika kozi hiyo na jumla ya wahitimu 489 wa ngazi ya cheti.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Champions League – Team news: RVP in squad

Wanafunzi wafanya Vizuri katika Michezo Dar..