in ,

RVP-Nahodha mpya Arsenal FC….

Robin van Persie

Robin van Persie

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 28 anayechezea pia timu ya taifa ya Uholanzi, amekuwa katika klabu ya Arsenal tangu mwezi wa Mei mwaka 2004 na anachukua nafasi hiyo kutoka kwa Cesc Fabregas, aliyehamia klabu ya Barcelona wiki hii.

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema: “Van Persie ni kiongozi kutokana na uchezaji wake, kutokana na ushawishi wake na ari aliyonayo ya kushinda.
“Amekuwa aktika klabu hii kwa muda mrefu na kiufundi ni kiongozi.”
Van Persie, ambaye msaidizi wake anakuwa mlinzi Thomas Vermaelen, amesema amefurahia kupata nafasi hiyo.

“Kuwa nahodha, unakuwa ni balozi kwa klabu na nipo tayari kwa hilo,” amesema Van Persie. “Nimekuwa katika soka kwa zaidi ya miaka 10, kwa hiyo naelewa namna ya kutekeleza majukumu yangu.

“Kila mara unalazimika kuonesha heshima mbele za watu.
Van Persie hataiongoza Arsenal katika mechi dhidi ya Udinese usiku wa Jumanne katika kuwania nafasi ya kufuzu mechi za Ubingwa wa Ulaya, kwa sababu anatumikia adhabu ya kufungiwa mechi moja na Uefa.

Lakini atachukua hatamu za kuiongoza Arsenal watakapomenyana na Liverpool katika uwanja wa Emirates siku ya Jumamosi kwenye pambano la Ligi Kuu ya Soka ya England.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Gervas Kago, ruksa kuichezea SSC

TFF bows to Simba claim