in

Ngassa afanya majaribio na West Ham

Mshambuliaji wa pembeni wa Yanga na timu ya taifa, Taifa Stars, Mrisho Ngassa (Pichani), ameanza majaribio yake juzi kwenye klabu ya West Ham United ya Uingereza akiwa na hofu kutokana na kukutana na idadi kubwa ya wachezaji waliokwenda kufanya majaribio kwenye klabu hiyo.

_ngasa

Ngassa, ambaye alitua nchini Uingereza mwanzoni mwa wiki hii, alianza rasmi mazoezi akiwa na kikosi cha pili cha timu hiyo kilichochanganywa na wachezaji hao wanaojaribiwa, ambapo hali hiyo ilimfanya Ngassa kucheza kwa kutojiamini hali iliyosababisha wakala wake Yusuph Bakhresa kumtuliza presha.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo Nipashe imezipata kutoka kwa Bakhresa, imeelezwa kuwa siku ya kwanza ya majaribio yake Ngassa, hakuonyesha uwezo wake kutokana na kuwa na hofu hasa baada ya kuona idadi ya wanaofanyiwa majaribio ni kubwa.

Imeleezwa kuwa baada ya hali ile Bakhresa, alimtaka mchezaji huyo kucheza soka lake la kawaida na kuondoa hofu ushauri ambao aliutekeleza, ambapo jana alifanya mazoezi ya pamoja na kikosi cha kwanza cha West Ham.

Taarifa hiyo imeweka wazi kuwa baada ya ushauri huo Ngassa, alitulia na kucheza mpira wake wa kawaida, ambapo juzi alionyesha uwezo uliompa nafasi ya kujumuika na kikosi cha kwanza cha West Ham.

“Kidogo alipata wasiwasi katika siku ya kwanza ya majaribio yake, lakini aliwekwa sawa na sasa anaendelea vizuri na anaonyesha mchezo wake wa kawaida,”alisema Bakhresa.

Mchezaji huyo ataendelea kufanya majaribio na kikosi cha kwanza hadi pale atakapomaliza muda uliopangwa kwa ajili ya majaribio hayo.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply
  1. Ngasa akitulia atafanya vizuri na kushinda majaribio hayo ,kiwango anacho cha kucheza mpira kokote duniani ,hivyo kila la heri ngasa ,kwani hiyo itakuwa ni mafanikio ya taifa na kutangaza soka la tz.Wadau tumtakie kiujumla la heri sio kutuma maoni kiushabiki ,kisimba.Big j

  2. ngasa ajitaidi anao uwezo,atangaze tanzania kuwa ina vipaji iyo ndiyo njia yakupeleka tanzania kombe la dunia.kujiamini ndio njia pekee

  3. Ngassa jitahidi mzee Watanzania wote tunakupmbea. Hakika hakuna kinachoshindikana chini ya jua.

  4. nadhani ma agent wetu waanzie vilabu vya chini kama ilivyokua lov ham lakini akabaniwa kwa west ham naona ni ngumu ila mungu ndiye anaejua tusubiri ijumaa hii kitajulikana.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Wenger transfer policy under fire

Fabregas – Trophy would be dream come true