in , , ,

Morocco: Uenyeji Kombe la Dunia ngoma inanoga




MATUMAINI ya Morocco kuandaa fainali za Kombe la Dunia 2026 yamezdi 
kuongezeka, huku ikidhaniwa kwamba kuna wanachama wa Shirikisho la 
Soka la Kimataifa (Fifa) kutoka Amerika ambao hawatapiga kura. 
Mchuano wa uenyeji wa fainali hizo umekuwa mkubwa, ambapo watu walio 
ndani ya Fifa wanasema kwamba Morocco wanazidi kupewa nafasi kadiri 
muda unavyokwenda.


Wakipata watakuwa nchi ya pili Afrika kuandaa fainali hizo baada ya 
Afrika Kusini. Wanachuana na muungano wa mataifa ya Amerika – 
Marekani, Mexico na Canada wanaotaka kuandaa kwa pamoja. 
Hapana ubishi kwamba mataifa hayo matatu kuwa wenyeji kunaweza 
kuonekana kwamba ni mbadala salama zaidi na wneye kuvutia kifedha 
lakini hiyo haitoshi kuwahakikishia kura kutoka kwa mashirikisho 
wanachama wa Fifa.
 

Nafasi yao ya kushinda kete hii ya uenyeji ilidhaifishwa kwa sababu ya 
kuibuka kwa mzozo miongoni mwa himaya za Marekani za Guam, Puerto 
Rico, American Samoa na US Virgin Islands kutokana na mgongano wa 
kimaslahi. 

Hii ni kura ya kwanza kwa ajili ya uenyeji wa fainali za Kombe la 
Dunia tangu England walipopatwa pigo kubwa kwa kushindwa kupata 
uenyeji wa fainali za mwaka huu wakati Urusi na Qatar walipochaguliwa 
kuwa wenyeji wa 2018 na 2022 licha ya kuonekana dhaifu kinadharia 
kwenye karatasi.

Tuhuma na shutuma nyingi juu ya rushwa kwenye shirikisho hilo katika 
kupata wenyeji hao na mabadiliko makubwa ya kiungozi na hata viongozi 
kukamatwa na kushitakiwa kwa rushwa, kunaonesha kwamba mambo yatakuwa 
tofauti sana safari hii na uwazi utatawala. 

Inatarajiwa kwamba mashirikisho wanachama 201 kati ya 211 watapiga 
kura kwenye mkutano wa mwaka wa baraza la Fifa unaofanyika leo 
Jumatano Expocentre, Moscow.
 

Mataifa manne yanayowania uenyeji hayatapiga kura wakati Ghana na 
Kosovo wanajulikana kwamba hawakutuma mwakilishi. Serikali ya Ghana 
imevunjilia mbali shirikisho la soka la nchi hiyo kutokana na sababu 
za rushwa kukithiri humo.
 

Wakuu wa Fifa, akiwamo Rais Gianni Infantino – wanatambulika kwamba 
wangependa kuona maombi ya Marekani na washirika wake yakikubaliwa kwa 
kura, maana wameahidi (waandaaji) kwamba yakifanyika humo yatazalisha 
faida ya pauni bilioni 8.1 ikilinganishwa na ya pauni bilioni 4.4.

inayotarajiwa kupatikana iwapo mashindano yatafanyika Morocco. Hata 
hivyo, kuna sababu nyingine za kijiografia, kisiasa na kisoka za 
kuzingatia kabla ya uamuzi kuchukuliwa.
 

Baadhi ya watu wanaopendelea maombi ya muungano wa nchi hizo za 
Amerika wana wasiwasi kwamba kuingilia kwenye kampeni kwa Rais Donald 
Trump wa Marekani kunaweza kuwa kumewaharibia.
 

Aprili mwaka huu aliandika kwenye ukurasa wake wa mtandao wa jamii wa 
Twitter akisema; “Marekani imeweka kwa pamoja ombi zito na Canada na 
Mexico kwa ajili ya fainali za Kombe la Dunia 2026. Itakuwa fedheha 
iwapo nchi tunazozisaidia siku zote zitafanya kampen dhidi ya ombi la 
Marekani. Kwa nini tuwe tunazisaidia nchi hizi ikiwa hazishirikiani 
nasi (pamoja na Umoja wa Mataifa)?” 

Ni maoni ya baadhi ya watu kwamba utata wake unaweza kusababisha 
baadhi ya mataifa kuamua kuwapinga na kwenda na Morocco. Lakini pia 
mzozo ulioibuka baina ya Trump na Waziri Mkuu wa Canada, Justin 
Trudeau kunaweza kufisha nguvu ya ushirika wa waandaaji wenza hao.

Hata hivyo, inadaiwa kwamba nyuma ya pazia Trump amekuwa akipiga 
kampeni, ikiwa ni pamoja na kuandika barua tatu kwa Infantino na 
maofisa wengine wa Fifa, akiwahakikishia kwamba msimamo wake mkali 
hautaathiri masuala ya visa kwa wageni kuingia Marekani. 

Pamoja na hayo, jopo la wana kampeni wa Morocco kwa ajili ya kuandaa 
mashindano hayo walikuwa na imani kwamba wangeweza kubadili mawazo ya 
baadhi ya nchi wanachama wa Fifa na kuwaunga wao mkono.


Walikuwa wakiendelea na kampeni hizo kwenye vyumba na korido za hoteli 
mbalimbali na baa jijini Moscow hadi muda wa mwisho ukikaribia. 
Watakuwa na muda wa dakika 15 kwa ajili ya kuwasilisha mada mbele ya 
baraza leo asubuhi kushawishi wajumbe ili wapate kura.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

UJERUMANI WATAFANIKIWA KUTETEA KOMBE LAO?

Tanzania Sports

MESSI NA ARGENTINA HAWATAFIKA MBALI RUSSIA