in

Mkwasa: Kipigo 6-0 Twiga Stars kimetufunza

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya soka ya wanawake, Twiga Stars, Boniface Mkwasa, amesema kuwa licha ya timu yake kupokea kichapo cha 6-0 kutoka kwa wenzao wa Afrika Kusini, Banyana Banyana, timu hiyo imefaidika kiufundi na mechi hiyo ya kirafiki ya kimataifa.

Mkwasa amesema kuwa makosa waliyoyafanya wachezaji wake katika mechi hiyo, yamemsaidia kufahamu mapungufu waliyonayo na sasa ataelekeza nguvu katika kuyafanyia kazi ili kuimarisha kikosi hicho kabla ya muda wa fainali za Mataifa ya Afrika kwa wanawake haujafika.

Mkwasa alisema kuwa anaamini baada ya kuyafanyia kazi mapungufu aliyoyaona, pamoja na kambi watakayoenda kuweka nchini Marekani, wachezaji wake watakuwa wamepata uzoefu wa kutosha na wataenda katika fainali hizo nchini Afrika Kusini wakiwa wameiva.

Alisema kuwa atafurahi kuona Twiga Stars inapata mechi nyingine ya kirafiki ya kimataifa na timu ngumu ili kupata uzoefu wa kukabiliana na ‘vigogo’.

Twiga Stars imefuzu kucheza fainali hizo kwa mara ya kwanza baada ya kuzifunga timu za Ethiopia na Eritrea na ushindi wa magoli 8-1, ambao iliupata dhidi ya Eritrea hapa nyumbani ndio uliwavutia Banyana Banyana na kuwaalika.

CHANZO: NIPASHE

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply
  1. kweli sio mbaya ni kujifunza sasa na kule tukikutana nao si watatupatia za kutosha zaid ya hizo kwa nini tusiwe na ligi ya ukweliya timu za wanawake hata ya mwezi mmja tuu tuache kutoa visingizio kila siku

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

La Liga – Arsenal ‘won’t negotiate’ Fabregas sale

With the new season only days away, tanzaniasports looks at how all 20 Premier League clubs are shaping up. Who’s in and who’s out – and, most importantly, how they are coping with the new squad rule of a maximum 25, with eight of those having to be home grown…