Menu
in , , ,

Man U wakwama Sunderland

Manchester United wameshindwa kutoka kwenye mtanziko wa kuanza vibaya ligi kuu.

Vijana wa Louis van Gaal wameambulia sare ya 1-1 nyumbani kwa Sunderland, na kumfanya Mdachi huyo aendelee kusubiri ushindi wake wa kwanza.

Juan Mata alitoa matumaini kwa kufunga bao dakika ya 17 lakini likafutwa na Jack Rodwell dakika 15 kabla ya mapumziko. Kadiri muda ulivyokwenda ufanisi wa Mata kwenye wingi ulipungua kwa kuzidiwa maarifa na Lee Cattermore na pia Nahodha Wayne Rooney hakufurukuta.                           

Mbaya zaidi, Ashley Young akishambulia ndani ya eneo la penati alijirusha, wakadai penati lakini akaishia kupewa kadi ya njano.  

Van Gaal na msaidizi wake, Ryan Giggs walizama katika majadiliano kuubadili mchezo ila itabidi waridhike na pointi moja waliyopata kwani walikuwa kikawaida sana.  Itabidi Man u wajitahidi kusajili wachezaji wengine wazuri.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version